Masomo Kutokana na Maandiko: Maombolezo 1:1–5:22
Yehova Hutoa Tumaini Katikati ya Majonzi
YEHOVA ndiye “Mungu ambaye hupa tumaini,” hata katikati ya majonzi. (Warumi 15:13, NW) Hili ni wazo linaloeleweshwa wazi katika kitabu cha Maombolezo, kilichokamilishwa na Yeremia mnabii na shahidi wa Yehova katika 607 K.W.K. Lakini acheni tukazie baadhi ya masomo kilicho nayo.
Shida Kubwa ya Yerusalemu
Dhambi haileti shangwe yo yote. Tazama! Yerusalemu wenye dhambi, uliokuwa mji mkuu wa Yuda wenye kumiminika watu wakati mmoja, umeketi upweke. Yuda yenyewe ni kama binti-mfalme mwenye machozi, aliyeachwa mjane kwa sababu imeachwa ukiwa. “Wapenzi” kama vile Misri hawakuiokoa isipate ushinde kutokana na Babuloni katika 607 K.W.K. Watu hawatiririki tena kwenda Sayuni kwa ajili ya sikukuu. Watoto wayo ni watekwa, na maadui wanacheka juu ya kuanguka kwayo. Watu wa kigeni wasio safi wametakatua utakatifu wa hekalu, na watu wayo wamelazimika kutoa vitu vya kuthamanika ndipo wapewe chakula. Yote haya kwa sababu ya dhambi!—1:1-11.
Yehova ni mwadilifu katika kuadhibu watenda makosa. Jambo hilo linakubaliwa wazi wakati Yerusalemu wenyewe unaponena. Huo unauliza kama kuna majonzi yo yote yaliyo kama umivu ambalo Mungu ameusababishia. Yeye ali peleka moto ulioliacha hekalu ukiwa. Dhambi za jiji zilikuja kuwa nira, na damu ilichururika kama utomvu wa matunda huku Mungu akikanyaga-kanyaga “shinikizo-divai” lao. Sayuni ilitandaza mikono kwa majonzi na kusihi kwa kujitetea isipate mfariji, na Yehova alikuwa mwadilifu katika kuadhibu Yerusalemu wenye uasi. Yeye na ashughulike vikali hivyo hivyo kwa maadui wake wenye kuchachawa.—1:12-22, NW.
“Hasira-Kisasi ya Yehova”
Wenye madaraka wana hatia ikiwa hawa shutumu dhambi. Mungu alitupa Yerusalemu “kutoka mbinguni mpaka duniani,” akiruhusu uharibifu wao na ule wa “kibago-nyayo” chake, yaani hekalu. (Zaburi 132:7, NW) Hivyo yeye ‘alitweza utakato wa ufalme’ wa Yuda. Likiwa kama kibanda tu, hekalu liliharibiwa na maadui ambao makelele yao ya kushangilia ushindi yalikuwa kama vilio vya kisikukuu. Watoto wenye kufa waliwaomba mama zao kimaskini wawape chakula. Lakini ni nani hasa aliyekuwa na hatia kubwa? Ni wanabii bandia waliotoa matamko rasmi yenye kuongoza watu vibaya badala ya kushutumu dhambi ya Yerusalemu. (Yeremia 14:13, NW) Sala inafaa, kwa maana wengi sana wamekufa katika hii ‘siku ya hasira-kisasi ya Yehova’!—2:1-22, NW.
Rehema ya Yehova inadumu
Inatupasa sisi tutumaini katika Yehova kwa saburi. Yeremia anaonyesha wazo hilo anaponena kwa kuwakilisha wale watu wenye kusumbuka. Mungu anaweka mgogoro kuzuia sala yake, na yeye amekuwa kichwa kikuu cha wimbo wa kuchekwa kimadharau na adui zake. Tumaini lake, au “tarajio kutoka kwa Yehova,” linaonekana ni kama limetoweka. Lakini yeye atakuwa na “mwelekeo wa kungojea” kwa sababu “Yehova ni mwema kwa mmoja ambaye anatumaini katika yeye.”—3:1-27, NW.
Toba ya kweli yaleta rehema ya kimungu. Kwa kusadiki jambo hilo, Yeremia anahimiza hivi: “Acheni sisi turudi moja kwa moja kwa Yehova.” Kama kwamba kwa kutumia tungamo la wingu la kasirani, Mungu amezuia ukaribiwa katika sala kwa sababu ya dhambi za wale watu. Lakini Yeremia anasali hivi: “Mimi nimeita jina lako kwa kupaaliza sauti, O Yehova. . . . Usifiche sikio lako kwa liwazo langu.” Bila shaka, maadui wasiotubu wataangamizwa kabisa.—3:28-66, NW.
“Turudishe”
Sisi tunaweza kuleta uharibifu juu yetu wenyewe kupitia dhambi ya kutendwa kwa makusudi. Kwa sababu ya dhambi ya Yuda, “wana wenye thamani kubwa wa Sayuni” walionwa kuwa kama chungu kilichovunjwa kisichostahiki kitu. Katika yale mazingiwa, wale waliochinjwa na upanga walikuwa afadhali sana kuliko wengine wenye kufa polepole kutokana na njaa. Kweli kweli, Mungu alikuwa ‘amemimina kasirani yake inayowaka.’ Wanabii na makuhani waliotiwa uchafuzi walikuwa wakitangatanga kiupofu, na Mfalme Sedekia—“yule mmoja mpakwa-mafuta wa Yehova”—alikuwa ametekwa. Sasa Mungu angegeuza fikira zake kwenye Edomu wenye dhambi.—4:1-22, NW.
Yehova peke yake ndiye hutoa tumaini la kweli katikati ya majonzi. Yeremia aling’amua jambo hilo, kwa maana yeye alisihi hivi kwa kutetea: “Kumbuka, O Yehova, jambo lililotukia kwetu.” ‘Watu wa kigeni wanakaa nyumba zetu. Sisi tunayahimili matokeo ya kosa la baba zetu wa kwanza, na vivulana tu wanabeba kuni katika kazi-jasho ya kulazimishwa.’ Hata hivyo, Yeremia anatumainia rehema, akisali hivi: “Turudishe, O Yehova, kwako wewe mwenyewe, na sisi tutarudi kwa utayari.”—5:1-22, NW.
Basi, fikiria masomo haya yanayofundishwa katika Maombolezo: Dhambi haileti shangwe yo yote, Mungu ni mwadilifu katika kuadhibu watenda dhambi, na wenye madaraka wana hatia ikiwa hawashutumu utendaji makosa. Inatupasa sisi tutumaini katika Yehova kwa saburi, tukiwa na uhakika kwamba rehema ya kimungu inakuja kwa sababu ya toba ya kweli, hali sisi tunaweza kuleta uharibifu juu yetu wenyewe kupitia dhambi ya makusudi. Kitabu hiki kilichovuviwa kinatusadikisha pia kwamba Yehova ndiye peke yake hutoa tumaini la kweli katikati ya majonzi.
[Sanduku katika ukurasa wa 27]
MAANDIKO YA BIBLIA YACHUNGUZWA
◻ 1:15, NW—‘Yehova alikuwa amekanyaga-kanyaga shinikizo-divai lenyewe lililokuwa la binti bikira wa Yuda’kwa sababu Yehova alikuwa ameamua na kuruhusu lililotukia. “Binti bikira wa Yuda” alikuwa Yerusalemu, uliofikiriwa kuwa kama mwanamke asiyenajisiwa. Wakati Wababuloni walipoharibu jiji hilo kuu la Yuda katika 607 K.W K., kulikuwa na umwagaji mkubwa wa damu, unaolinganika na kukamua umaji-maji wa matunda-zabibu katika shinikizo-divai. Yehova atahakikisha kwamba Jumuiya ya Wakristo, Yerusalemu ulio kifananishwa, utapondwa-pondwa vivyo hivyo
◻ 2:6, NW—“Kibanda” cha Mungu kilikuwa hekalu katika Yerusalemu Wakati patakatifu hapo palipoteketezwa na Wababuloni, yeye alikuwa akiparuhusu ‘patendewe kwa jeuri,’ kama kijumba cha kuezekwa tu katika bustani Kifichio hicho cha muda tu chenye kukinga na jua kali kinabomolewa
◻ 3:16, NW—Afa moja ambalo Yehova aliruhusu lije juu ya Yerusalemu usio mwaminifu kwa kuangushwa kwa jiji hilo na Wababuloni linasimuliwa katika maneno haya, “Kwa vijiwe-jiwe yeye afanya meno yangu yavunjike” Inaonekana kwamba, wakati Waisraeli walipokuwa njiani kuingia uhamishoni, walilazimika kuoka mkate katika mashimo yaliyochimbwa katika ardhi Kwa hiyo, mkate huo ukaja kuwa na changarawe, na mtu mwenye kula mkate huo angeweza kukatika sehemu ya meno yake.
◻ 4:3, NW—Ukatili wa akina mama kuelekea watoto wao unatofautishwa hapa na ule utunzaji wa kimama unaoandaliwa na majibwa-mwitu. Ingawa huenda majibwa-mwitu yakaonwa kuwa ni hayawani wakali, hata wao‘wanatokeza kiwele na kunyonyesha watoto wao.’ Kwa sababu ya upungufu mkubwa wa vyakula katika Yerusalemu wenye kuzingiwa, wanawake Wayahudi wenye njaa kali walikuja kuwa wakatili katika jambo la kwamba hawakuwa na maziwa ya kuwapa wazao wao na kwa kweli walikula watoto wao wenyewe ili wao wabaki wakiwa hai. (Maombolezo 2:20) Hivyo, wanawake hao walikuja pia kuwa kama mbuni wanaotaga mayai yao na kuyaachilia mbali.
◻ 5:7, NW—Wayahudi wa siku ya Yeremia walilazimika kuhimili makosa ya baba zao wa kwanza. lakini hiyo haimaamshi kwamba Yehova huadhibu watoto moja kwa moja kwa ajili ya dhambi za wazazi wao Kwa kweli, matokeo mabaya ya kutenda makosa huhisiwa na vizazi vya baadaye. (Yeremia 31:29, 30) Kwa hiyo inafaa tukumbuke kwamba ni lazima sisi binafsi tutolee Mungu hesabu.—Warumi 14:12.