-
“Yeye Ni Mwenye Hekima Moyoni”—Lakini MnyenyekevuMkaribie Yehova
-
-
3 Yehova ni mtakatifu. Kwa hiyo, hana sifa ya kiburi ambayo inamtia mtu unajisi. (Marko 7:20-22) Isitoshe, angalia maneno ambayo nabii Yeremia alimwambia Yehova: “Bila shaka nafsi yako [Yehova mwenyewe] itanikumbuka na kuniinamia.”a (Maombolezo 3:20, NW) Hebu wazia! Yehova, Bwana Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu, alikuwa tayari ‘kumwinamia,’ au kujinyenyekeza kufikia kiwango cha Yeremia. Alifanya hivyo ili kumpa uangalifu unaofaa mwanadamu huyo asiyekamilika. (Zaburi 113:7) Naam, Yehova ni mnyenyekevu. Lakini Mungu anaonyeshaje unyenyekevu? Unahusianaje na hekima? Na kwa nini unyenyekevu ni muhimu kwetu?
-
-
“Yeye Ni Mwenye Hekima Moyoni”—Lakini MnyenyekevuMkaribie Yehova
-
-
a Waandishi wa kale, au Wasoferi, walibadili mstari huu kusema kwamba ni Yeremia anayeinama wala si Yehova. Inaonekana kwamba walidhani haifai kusema kwamba Mungu alitenda kitendo hicho cha unyenyekevu. Ndiyo sababu tafsiri nyingi zinakosa maana ya mstari huu wenye kupendeza. Hata hivyo, The New English Bible inasema kwa usahihi kwamba Yeremia alimwambia Mungu hivi: “Kumbuka, Ee kumbuka, na uniinamie.”
-