-
‘Nafsi Yako Itainama Juu Yangu’Mnara wa Mlinzi—2012 | Juni 1
-
-
UNYENYEKEVU ni sifa yenye kuvutia. Mara nyingi sisi tunajihisi huru kuwakaribia watu wanyenyekevu. Hata hivyo, inasikitisha kwamba leo ni vigumu kupata watu wenye unyenyekevu wa kweli, hasa watu wenye nguvu na mamlaka kuliko wengine. Vipi kumhusu Yehova Mungu ambaye ana nguvu zaidi kuliko mtu yeyote yule? Je, Yeye ni mnyenyekevu? Acheni tuchunguze maneno ya nabii Yeremia yanayopatikana katika andiko la Maombolezo 3:20, 21.—Soma.
-
-
‘Nafsi Yako Itainama Juu Yangu’Mnara wa Mlinzi—2012 | Juni 1
-
-
Yeremia ana hakika kwamba Yehova ‘atainama’ juu ya wale wanaotubu kikweli. Tafsiri nyingine zinasema hivi: “Ee unikumbuke, na kujishusha chini kwangu.” Maneno hayo yanatusaidia kumwona Yehova kuwa mwenye fadhili. Yehova ‘aliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote,’ atajishusha chini katika njia ya mfano, na kuwainua waabudu wake kutoka katika hali yao mbaya na kuwakubali tena. (Zaburi 83:18) Kwa sababu ya kuimarishwa na tumaini hilo, Yeremia anapata faraja ya kweli kwa moyo wake uliokuwa umehuzunika. Nabii huyo mwaminifu ameazimia kungoja kwa subira hadi wakati unaofaa wa Yehova atakapowakomboa watu Wake wanaotubu.—Mstari wa 21.
-