-
“Sasa Mwisho Umekufikia”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
6. (a) Ezekieli aliwakilisha mambo gani mawili kwa wakati mmoja alipokuwa akiigiza? (b) Amri ya Mungu ya ‘kupima nywele na kuzigawa’ inamaanisha nini?
6 Kuharibiwa kwa Yerusalemu na watu wake. Katika sehemu hii ya unabii wa kuigiza, Ezekieli aliwakilisha mambo mawili kwa wakati mmoja. Kwanza, aliigiza jambo ambalo Yehova angefanya. Yehova alimwambia hivi Ezekieli: “Chukua upanga mkali ili uutumie kama wembe wa kinyozi.” (Soma Ezekieli 5:1, 2.) Mkono wa Ezekieli ulioshika upanga uliwakilisha mkono wa Yehova—hukumu ya Yehova—kama ilivyotekelezwa kupitia jeshi la Babiloni. Pili, Ezekieli aliigiza jambo ambalo lingewapata Wayahudi. Yehova alimwambia Ezekieli hivi: “Nyoa kichwa chako na ndevu zako.” Kunyolewa kwa kichwa cha Ezekieli kuliwakilisha jinsi ambavyo Wayahudi wangeshambuliwa na kuangamizwa. Pia, amri ya ‘kuzipima nywele hizo na kuzigawa katika mafungu’ kulimaanisha kwamba hukumu ya Yehova dhidi ya Yerusalemu haingetekelezwa ovyoovyo bali ingetekelezwa kwa makini na kikamili.
-
-
“Nyoa Kichwa Chako na Ndevu Zako”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
“Nyoa”
Wayahudi wangeshambuliwa na kuangamizwa
‘Pima na Kuzigawa’
Hukumu itatekelezwa kwa makini na kikamili
-