Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Sasa Mwisho Umekufikia”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Ezekieli ananyoa nywele na ndevu zake.

      SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 6A: “Nyoa Kichwa Chako Na Ndevu Zako”

      7. Kwa nini Yehova alimwambia Ezekieli azigawe nywele katika mafungu matatu na kulitendea kila fungu kwa njia tofauti?

      7 Kwa nini Yehova alimwambia Ezekieli azigawe nywele zake katika mafungu matatu na kulitendea kila fungu jambo tofauti? (Soma Ezekieli 5:7-12.) Ezekieli alichoma sehemu moja ya nywele “ndani ya jiji” kuwaonyesha watazamaji kwamba baadhi ya wakaaji wa Yerusalemu wangekufa jijini. Ezekieli aliipiga sehemu nyingine ya nywele kwa upanga “kulizunguka jiji pande zote” kuonyesha kwamba wakaaji wengine wangeuawa nje ya jiji. Aliitawanya hewani sehemu ya mwisho ya nywele kuonyesha kwamba bado wakaaji wengine wangetawanyika miongoni mwa mataifa, lakini “upanga” ‘ungewakimbiza.’ Hivyo, popote pale ambapo waokokaji hao wangeishi, hawangepata amani.

  • “Nyoa Kichwa Chako na Ndevu Zako”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
      • Ezekieli achoma baadhi ya nywele zake.

        ‘Teketeza’

        Baadhi ya watu wangekufa jijini

      • Ezekieli apiga baadhi ya nywele zake kwa upanga.

        ‘Piga kwa Upanga’

        Baadhi ya watu wangeuawa nje ya jiji

      • Ezekieli atawanya baadhi ya nywele zake kwenye upepo.

        ‘Tawanya’

        Baadhi ya watu wangeponyoka, lakini hawangepata amani

  • “Sasa Mwisho Umekufikia”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 10 Neno la Mungu linaonyesha kwamba wafuasi mmoja-mmoja wa dini ya uwongo wataokoka dini za uwongo zitakapoharibiwa. Wakiwa na hofu, waokokaji hao wataungana na watu wengine watakaokuwa wakitafuta mahali pa kujificha. (Zek. 13:4-6; Ufu. 6:15-17) Hali yao inatukumbusha jambo lililowapata wakaaji wa Yerusalemu la kale ambao waliokoka lilipoharibiwa na kutawanyika “kwenye upepo.” Kama tulivyoona katika fungu la 7, ingawa kwa muda fulani uhai wao uliokolewa, Yehova alichomoa “upanga ili kuwakimbiza.” (Eze. 5:2) Vivyo hivyo, mahali popote ambapo waokokaji wa shambulio dhidi ya dini huenda wakakimbilia hawatalindwa kutokana na upanga wa Yehova. Wakati wa Har–Magedoni, watauawa, pamoja na wale wote walio kama mbuzi.— Eze. 7:4; Mt. 25:33, 41, 46; Ufu. 19:15, 18.

      Kuhusu kuhubiri habari njema, tutakuwa “bubu”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki