Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Nitawapa Moyo Wenye Umoja”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 11 Katika kipindi chote cha giza la utawala wa dini zinazodai kuwa za Kikristo, kulikuwa na baadhi ya Wakristo wa kweli, “ngano” ambayo Yesu alitaja kwenye mfano wake. Kama Wayahudi waliokuwa uhamishoni wanaotajwa katika Ezekieli 6:9, walimkumbuka Mungu wa kweli. Baadhi yao walipinga kwa ujasiri mafundisho ya uwongo ya dini zinazodai kuwa za Kikristo. Walidhihakiwa na kuteswa. Je, Yehova alikusudia kuwaacha watu wake katika giza hilo la kiroho milele? Hapana! Kama ilivyokuwa kwa Waisraeli wa zamani, Yehova alionyesha hasira kwa kiwango kinachofaa na kwa kipindi kinachofaa cha wakati. (Yer. 46:28) Isitoshe, Yehova hakuwaacha watu wake bila tumaini. Acheni tuzungumzie tena wale Wayahudi waliokuwa uhamishoni katika Babiloni la kale na tuone jinsi Yehova alivyowapa tumaini la kuwatoa utekwani.

      Makasisi wakijitayarisha kumchoma kwenye mti Mkristo wa kweli katika enzi za giza la dini zinazodai kuwa za Kikristo.

      Kwa karne nyingi, Wakristo wa kweli walikabili mateso mikononi mwa Babiloni Mkubwa (Tazama fungu la 10, 11)

  • “Nitawapa Moyo Wenye Umoja”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 13 Kati ya mateka kulikuwa na Wayahudi waaminifu waliopelekwa uhamishoni pamoja na watu wasio waaminifu. Isitoshe, kupitia Ezekieli, Mungu alitabiri kwamba baadhi ya watu wake wangetubu wakiwa uhamishoni. Wayahudi hao waliotubu wangesimulia mambo ya kuaibisha ambayo walifanya walipomwasi Mungu wao, nao wangemwomba Yehova msamaha na kibali. (Eze. 6:8-10; 12:16) Ezekieli, nabii Danieli na wenzake watatu, walikuwa miongoni mwa watu hao waaminifu. Danieli aliishi muda mrefu hivi kwamba aliona mwanzo na mwisho wa uhamisho. Sala yake ya kutoka moyoni ya kutubu dhambi za Israeli imeandikwa katika Danieli sura ya 9. Bila shaka, maneno yake yaliwakilisha hisia za maelfu ya watu waliokuwa uhamishoni ambao walitamani kusamehewa na Yehova na kupata baraka tena. Walichochewa sana na ahadi za Ezekieli zilizoongozwa na roho kuhusu kuwekwa huru na kurudishwa katika nchi yao!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki