Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Ona Mambo Maovu na Yenye Kuchukiza Wanayofanya’
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Tukio la Pili: Wazee 70 Wakiitolea Miungu ya Uwongo Uvumba

      Ezekieli akitazama ndani ya ua wa ndani wa hekalu ambapo wazee wanafukizia uvumba mifano ya miungu ya uwongo iliyochongwa ukutani.

      11. Ezekieli aliona mambo gani yenye kuchukiza alipoingia katika ua wa ndani karibu na madhabahu ya hekalu?

      11 Soma Ezekieli 8:7-12. Ezekieli alipotoboa ukuta na kuingia katika ua wa ndani karibu na madhabahu ya hekalu, aliona michoro yenye kuchukiza ya “viumbe wanaotambaa na wanyama wanaochukiza na sanamu zote zinazochukiza.”c Michoro hiyo iliyokuwa ukutani iliwakilisha miungu ya uwongo. Kisha jambo ambalo Ezekieli aliona lilikuwa lenye kuchukiza sana: “Wazee 70 wa nyumba ya Israeli” walikuwa wamesimama “gizani” wakiitolea miungu ya uwongo uvumba. Chini ya Sheria, kufukiza uvumba wenye harufu tamu kuliwakilisha sala zilizokubaliwa ambazo zilitolewa na waabudu waaminifu. (Zab. 141:2) Hata hivyo, uvumba ambao wale wazee 70 waliitolea miungu ya uwongo ulikuwa uvundo mchafu kwa Yehova. Sala zao zilikuwa kama harufu mbaya inayomchukiza. (Met. 15:8) Wazee hao walijidanganya hivi: “Yehova hatuoni.” Lakini Yehova aliwaona, na alimwonyesha Ezekieli mambo ambayo hasa walikuwa wakifanya katika hekalu lake!

      Wazee sabini wanafukizia uvumba mifano ya miungu ya uwongo iliyochongwa ukutani.

      Yehova anaona kila jambo lenye kuchukiza linalofanywa “gizani” (Tazama fungu la 11)

      12. Kwa nini tunapaswa kuendelea kuwa waaminifu “gizani,” na ni nani hasa wanapaswa kuweka mfano mzuri katika jambo hilo?

      12 Tunaweza kujifunza nini kutokana na simulizi la Ezekieli kuhusu wale wazee 70 Waisraeli walioitolea miungu ya uwongo uvumba? Ili Mungu asikilize sala zetu na ibada yetu iwe safi machoni pake, tunapaswa kuendelea kuwa waaminifu hata tukiwa “gizani.” (Met. 15:29) Acheni tukumbuke kwamba sikuzote Yehova anaona kila kitu tunachofanya. Ikiwa Yehova ni halisi kwetu, hatutafanya jambo lolote faraghani ambalo tunajua halimpendezi. (Ebr. 4:13) Hasa wazee wa kutaniko wanapaswa kuweka mfano mzuri katika kufuata kanuni za Biblia. (1 Pet. 5:2, 3) Washiriki wa kutaniko wanatazamia kwamba mzee anayesimama mbele yao na kuwaongoza katika ibada mikutanoni anaishi kulingana na kanuni za Biblia hata akiwa “gizani,” yaani, wakati wengine hawamwoni.—Zab. 101:2, 3.

  • ‘Ona Mambo Maovu na Yenye Kuchukiza Wanayofanya’
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • “Mwana wa Binadamu, Je, Unaona Hili?”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • ‘Ona Mambo Maovu na Yenye Kuchukiza Wanayofanya’
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Tukio la Pili: Wazee 70 Wakiitolea Miungu ya Uwongo Uvumba

      Ezekieli akitazama ndani ya ua wa ndani wa hekalu ambapo wazee wanafukizia uvumba mifano ya miungu ya uwongo iliyochongwa ukutani.

      11. Ezekieli aliona mambo gani yenye kuchukiza alipoingia katika ua wa ndani karibu na madhabahu ya hekalu?

      11 Soma Ezekieli 8:7-12. Ezekieli alipotoboa ukuta na kuingia katika ua wa ndani karibu na madhabahu ya hekalu, aliona michoro yenye kuchukiza ya “viumbe wanaotambaa na wanyama wanaochukiza na sanamu zote zinazochukiza.”c Michoro hiyo iliyokuwa ukutani iliwakilisha miungu ya uwongo. Kisha jambo ambalo Ezekieli aliona lilikuwa lenye kuchukiza sana: “Wazee 70 wa nyumba ya Israeli” walikuwa wamesimama “gizani” wakiitolea miungu ya uwongo uvumba. Chini ya Sheria, kufukiza uvumba wenye harufu tamu kuliwakilisha sala zilizokubaliwa ambazo zilitolewa na waabudu waaminifu. (Zab. 141:2) Hata hivyo, uvumba ambao wale wazee 70 waliitolea miungu ya uwongo ulikuwa uvundo mchafu kwa Yehova. Sala zao zilikuwa kama harufu mbaya inayomchukiza. (Met. 15:8) Wazee hao walijidanganya hivi: “Yehova hatuoni.” Lakini Yehova aliwaona, na alimwonyesha Ezekieli mambo ambayo hasa walikuwa wakifanya katika hekalu lake!

      Wazee sabini wanafukizia uvumba mifano ya miungu ya uwongo iliyochongwa ukutani.

      Yehova anaona kila jambo lenye kuchukiza linalofanywa “gizani” (Tazama fungu la 11)

      12. Kwa nini tunapaswa kuendelea kuwa waaminifu “gizani,” na ni nani hasa wanapaswa kuweka mfano mzuri katika jambo hilo?

      12 Tunaweza kujifunza nini kutokana na simulizi la Ezekieli kuhusu wale wazee 70 Waisraeli walioitolea miungu ya uwongo uvumba? Ili Mungu asikilize sala zetu na ibada yetu iwe safi machoni pake, tunapaswa kuendelea kuwa waaminifu hata tukiwa “gizani.” (Met. 15:29) Acheni tukumbuke kwamba sikuzote Yehova anaona kila kitu tunachofanya. Ikiwa Yehova ni halisi kwetu, hatutafanya jambo lolote faraghani ambalo tunajua halimpendezi. (Ebr. 4:13) Hasa wazee wa kutaniko wanapaswa kuweka mfano mzuri katika kufuata kanuni za Biblia. (1 Pet. 5:2, 3) Washiriki wa kutaniko wanatazamia kwamba mzee anayesimama mbele yao na kuwaongoza katika ibada mikutanoni anaishi kulingana na kanuni za Biblia hata akiwa “gizani,” yaani, wakati wengine hawamwoni.—Zab. 101:2, 3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki