Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mwana wa Binadamu, Je, Unaona Hili?”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • ‘Ona Mambo Maovu na Yenye Kuchukiza Wanayofanya’
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Tukio la Tatu: “Wanawake . . . Wakimlilia Mungu Tamuzi”

      Wanawake wakimlilia mungu Tamuzi.

      13. Ezekieli aliona wanawake walioasi imani wakifanya nini kwenye lango moja la hekalu?

      13 Soma Ezekieli 8:13, 14. Baada ya kuona matukio mawili ya mazoea yenye kuchukiza, Yehova alimwambia tena Ezekieli: “Utaona mambo yanayochukiza yaliyo mabaya hata zaidi ambayo wanafanya.” Basi, nabii huyo aliona nini kingine? Kwenye “lango la kaskazini la nyumba ya Yehova,” aliona “wanawake wameketi wakimlilia mungu Tamuzi.” Tamuzi, mungu wa Mesopotamia, anaitwa Dumuzi katika maandishi ya Kisumeria na inaaminiwa kwamba ni mpenzi wa mungu wa kike wa uzazi, Ishtari.d Inaonekana wanawake Waisraeli walikuwa wakilia kama sehemu ya desturi ya kidini iliyohusiana na kifo cha Tamuzi. Kwa kumlilia Tamuzi katika hekalu la Yehova, wanawake hao walikuwa wakifanya desturi ya kipagani katika kituo cha ibada safi. Lakini kushiriki ibada ya uwongo katika hekalu la Mungu hakukufanya ibada hiyo ya uwongo iwe safi. Kwa kuwa kulingana na maoni ya Yehova, wanawake hao walioasi imani walikuwa wakifanya “mambo yanayochukiza”!

      14. Tunajifunza nini kutokana na maoni ya Yehova kuhusu mambo ambayo wanawake walioasi imani walikuwa wakifanya?

      14 Tunajifunza nini kutokana na maoni ya Yehova kuhusu mambo ambayo wanawake hao walikuwa wakifanya? Ili ibada yetu iwe safi, hatupaswi kamwe kuichanganya na mazoea machafu ya kipagani. Basi tunapaswa kuepuka kabisa desturi zinazotokana na dini za kipagani. Je, ni muhimu kuchunguza chanzo? Ndiyo! Leo, desturi zinazohusiana na sherehe fulani, kama vile Krismasi na Ista, huenda zikaonekana kuwa hazina madhara. Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba Yehova alijionea mazoea ya dini za kipagani ambayo hatimaye yamekuwa sherehe za kisasa. Yehova hayakubali mazoea ya kipagani kwa sababu tu watu wameyafanya kwa muda mrefu au wameyachanganya na ibada safi.—2 Kor. 6:17; Ufu. 18:2, 4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki