-
“Uyatie Alama Mapaji ya Nyuso”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
7, 8. Wanaume waliokuwa na silaha za kuponda wangefanyaje kazi yao, na matokeo yalikuwaje?
7 Basi, wale wanaume sita wenye silaha za kuponda wangetimizaje kazi yao? Ezekieli alisikia maagizo ambayo Yehova aliwapa: Mfuateni mwanamume mwenye kidau cha wino na muue kila mtu isipokuwa mtu yeyote aliye na alama kwenye paji la uso. Yehova aliwaagiza hivi: “Mnapaswa kuanzia mahali pangu patakatifu.” (Eze. 9:6) Watekelezaji hao wa hukumu walipaswa kuanzia katikati ya Yerusalemu, katika hekalu, ambalo halikuwa tena takatifu mbele za Yehova. Kwanza, walipaswa kuwaua “wazee waliokuwa mbele ya ile nyumba”—wale wazee 70 wa Israeli waliokuwa hekaluni wakiifukizia uvumba miungu ya uwongo.—Eze. 8:11, 12; 9:6.
-
-
“Uyatie Alama Mapaji ya Nyuso”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
9, 10. Taja baadhi ya watu waliookoka uharibifu wa Yerusalemu, na tunaweza kusema nini kuwahusu?
9 Soma 2 Mambo ya Nyakati 36:17-20. Unabii wa Ezekieli ulitimizwa mwaka wa 607 K.W.K. jeshi la Babiloni lilipoharibu Yerusalemu na hekalu lake. Wababiloni walikuwa kama ‘kikombe mkononi mwa Yehova,’ ambacho alikitumia kumwaga adhabu juu ya jiji la Yerusalemu lililokosa uaminifu. (Yer. 51:7) Je, kila mtu aliuawa? Hapana. Maono ya Ezekieli yalikuwa yametabiri kwamba baadhi ya watu hawangeuawa na Wababiloni.—Mwa. 18:22-33; 2 Pet. 2:9.
10 Watu waaminifu waliokoka, kutia ndani Warekabu, Ebed-meleki Mwethiopia, Nabii Yeremia, na Baruku, mwandishi wake. (Yer. 35:1-19; 39:15-18; 45:1-5) Kulingana na maono ya Ezekieli, tunaweza kusema kwamba watu hao walikuwa “[wakilia] kwa uchungu na kwa maumivu makali kwa sababu ya mambo yote yanayochukiza” yaliyokuwa yakifanywa Yerusalemu. (Eze. 9:4) Bila shaka, kabla ya uharibifu walionyesha kwamba walichukia kabisa uovu na kwamba waliipenda ibada safi, na hivyo wakapata fursa ya kuokolewa.
11. Ni nani wanaowakilishwa na wanaume sita wenye silaha za kuponda na mwanamume mwenye kidau cha wino cha mwandishi?
11 Je, watu hao waaminifu walitiwa alama halisi ya kuokoka? Hakuna rekodi yeyote inayoonyesha kwamba mtu yeyote—iwe ni Ezekieli au nabii mwingine—alipita Yerusalemu na kutia alama halisi kwenye mapaji ya nyuso za watu waaminifu. Basi, inaonekana maono ya kinabii ya Ezekieli yanafunua mambo yaliyokuwa yakitokea mbinguni na hivyo hayangeonekana kwa macho ya kibinadamu. Mwanamume mwenye kidau cha wino cha mwandishi na wanaume sita wenye silaha za kuponda walikuwa mifano ya kinabii ya viumbe waaminifu wa kiroho wa Yehova, ambao sikuzote wako tayari kufanya mapenzi yake. (Zab. 103:20, 21) Bila shaka, Yehova aliwatumia malaika wake kutekeleza hukumu dhidi ya jiji la Yerusalemu lililokosa uaminifu. Kwa kuweka alama ya mfano kwenye mapaji ya nyuso za wale ambao wangeokolewa, malaika walihakikisha kwamba baadhi ya watu wangeokoka.
-