Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Nikaanza Kuona Maono ya Mungu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 15. Magurudumu ambayo Ezekieli aliona yalikuwa na ukubwa na muundo gani?

      15 Ezekieli alishangazwa na ukubwa wa magurudumu hayo. Aliandika hivi: “Mizingo yake ilikuwa juu sana hivi kwamba iliogopesha.” Tunaweza kuwazia Ezekieli akiinua kichwa chake kuangalia mizingo hiyo mikubwa inayong’aa na jinsi ilivyonyooka kuelekea mbinguni. Naye aliongezea maelezo haya yenye kustaajabisha: “Mizingo ya magurudumu yote manne ilikuwa imejaa macho kuizunguka.” Labda jambo la kushangaza zaidi lilikuwa umbo lisilo la kawaida la magurudumu hayo. Alieleza hivi: “Mwonekano wake na muundo wake ni kama gurudumu lililokuwa ndani ya gurudumu.” Hilo lilimaanisha nini?

  • “Nikaanza Kuona Maono ya Mungu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 17 Magurudumu yenye kimo kirefu hivyo yangeweza kukanyaga eneo kubwa sana hata kwa mzunguko mmoja tu. Kwa kweli, maono hayo yanaonyesha kwamba gari hilo lilisonga kwa mwendo kama radi! (Eze. 1:14) Zaidi ya hayo, wahandisi hawawezi kutengeneza magurudumu yenye uwezo kama huo wa kwenda pande zote nne. Gari hilo linaweza kwenda upande wowote bila kugeuka wala kupunguza mwendo! Hata hivyo, halifanyi hivyo bila kuona. Ni wazi kwamba macho yaliyojaa kuzunguka mizingo ya magurudumu yanaonyesha kwamba gari hilo linaona kila kitu pande zote.

      Magurudumu manne makubwa ya gari la kimbingu la Yehova.

      Magurudumu yalikuwa na ukubwa wa ajabu, na yalisonga kwa kasi sana (Tazama fungu la 17)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki