-
Unabii Kumhusu Masihi—Mwerezi MkubwaHatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
5. Chini ya kivuli cha utawala wa Ufalme wa Yesu, wanadamu watiifu wataishi kwa usalama
-
-
“Nitamweka Mchungaji Mmoja”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
10 Jinsi unabii huo unavyotimizwa. Yehova alimchukua mwana wake, Yesu Kristo kutoka kwenye ukoo wa kifalme wa Daudi (“mwerezi mkubwa”) na kumpanda juu ya Mlima Sayuni ulio mbinguni (“mlima mrefu na ulio juu sana”). (Zab. 2:6; Yer. 23:5; Ufu. 14:1) Kwa hiyo, Yehova alimchukua Mwana wake, ambaye alionwa na adui zake kuwa “mwanadamu wa hali ya chini zaidi” na kumkweza kwa kumpa “kiti cha ufalme cha Daudi baba yake.” (Dan. 4:17; Luka 1:32, 33) Kama mwerezi mkubwa, Mfalme wa Kimasihi Yesu Kristo atatawala dunia nzima na kuwaletea raia zake wote baraka. Kwa kweli, huyo ndiye Mtawala tunayepaswa kumtegemea. Chini ya kivuli cha utawala wa Ufalme wa Yesu, wanadamu waaminifu duniani kote ‘wataishi kwa usalama bila kuhangaishwa na woga wa msiba.’—Met. 1:33.
-