-
Dada Waliokuwa MakahabaHatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
Dada Waliokuwa Makahaba
Katika Ezekieli sura ya 23, watu wa Mungu wanashutumiwa vikali kwa sababu ya kukosa uaminifu. Sura hii inafanana kwa njia nyingi na sura ya 16. Kama sura ya 16, sura ya 23 inatumia mfano wa ukahaba. Yerusalemu ndiye dada mdogo, na Samaria ndiye dada yake mkubwa. Sura hizo mbili zinaonyesha jinsi dada mdogo alivyomwiga dada yake mkubwa akawa kahaba na akamzidi katika uovu na uasherati. Katika sura ya 23, Yehova anawapa majina dada hao wawili: Ohola ndiye dada mkubwa, yaani, Samaria, jiji kuu la ufalme wenye makabila kumi wa Israeli; Oholiba ndiye dada mdogo, yaani, Yerusalemu, jiji kuu la Yuda.a—Eze. 23:1-4.
-
-
Dada Waliokuwa MakahabaHatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
a Majina hayo yana maana. Ohola linamaanisha “Hema Lake [la Ibada]”—inaonekana linamaanisha hatua ya Israeli ya kuanzisha sehemu nyingine za ibada badala ya kumwabudu Yehova katika hekalu huko Yerusalemu. Kwa upande mwingine, Oholiba linamaanisha “Hema Langu [la Ibada] Liko Ndani Yake.” Yerusalemu lilikuwa kituo cha nyumba ya ibada ya Yehova.
-