-
“Nitamweka Mchungaji Mmoja”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
19 Unabii huo unasema nini? (Soma Ezekieli 34:22-24.) Mungu atamweka “mchungaji mmoja,” ambaye anamwita “mtumishi wangu Daudi.” Maneno “mchungaji mmoja” pamoja na neno “mtumishi” yanamaanisha kwamba Mtawala huyo hangeanzisha nasaba ya wafalme katika ukoo wa Daudi bali angekuwa mrithi pekee wa kudumu wa Daudi. Mtawala huyo aliye Mchungaji atawalisha kondoo wa Mungu na kuwa “kiongozi wao.” Yehova atafanya “agano la amani” pamoja na kondoo wake. “Baraka zitamwagika [juu yao] kama mvua,” nao watafurahia hali yenye kupendeza ya usalama, ufanisi, na kunawiri. Naam, kutakuwa na amani kati ya wanadamu na pia kati ya wanadamu na wanyama!—Eze. 34:25-28.
-
-
“Nitamweka Mchungaji Mmoja”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
19 Unabii huo unasema nini? (Soma Ezekieli 34:22-24.) Mungu atamweka “mchungaji mmoja,” ambaye anamwita “mtumishi wangu Daudi.” Maneno “mchungaji mmoja” pamoja na neno “mtumishi” yanamaanisha kwamba Mtawala huyo hangeanzisha nasaba ya wafalme katika ukoo wa Daudi bali angekuwa mrithi pekee wa kudumu wa Daudi. Mtawala huyo aliye Mchungaji atawalisha kondoo wa Mungu na kuwa “kiongozi wao.” Yehova atafanya “agano la amani” pamoja na kondoo wake. “Baraka zitamwagika [juu yao] kama mvua,” nao watafurahia hali yenye kupendeza ya usalama, ufanisi, na kunawiri. Naam, kutakuwa na amani kati ya wanadamu na pia kati ya wanadamu na wanyama!—Eze. 34:25-28.
-
-
“Nitamweka Mchungaji Mmoja”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
21 Maneno ya Ezekieli kuhusu “agano la amani” na mvua ya baraka yatakuwa na maana gani wakati ujao? Katika ulimwengu mpya unaokuja, waabudu wa kweli wa Yehova duniani watafurahia kikamili baraka za “agano la amani.” Katika paradiso halisi duniani kote, wanadamu waaminifu hawataogopa tena vita, uhalifu, njaa, magonjwa, au wanyama wa mwituni. (Isa. 11:6-9; 35:5, 6; 65:21-23) Je, huchochewi na tumaini la kuishi milele katika paradiso duniani ambako kondoo wa Mungu “wataishi kwa usalama, na hakuna mtu atakayewaogopesha”?—Eze. 34:28.
-