-
“Nitawafanya Kuwa Taifa Moja”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
3. (a) Kijiti “kwa ajili ya Yuda” kiliwakilisha nini? (b) Kwa nini “kijiti cha Efraimu” kiliwakilisha ufalme wenye makabila kumi?
3 Yehova alimwagiza Ezekieli achukue vijiti viwili na aandike juu ya kimoja “kwa ajili ya Yuda” na kingine “kwa ajili ya Yosefu, kijiti cha Efraimu.” (Soma Ezekieli 37:15, 16.) Vijiti hivyo viwili vilimaanisha nini? Kijiti ambacho kilikuwa “kwa ajili ya Yuda” kiliwakilisha ufalme wenye makabila mawili ya Yuda na Benjamini. Wafalme wa ukoo wa Yuda walitawala makabila hayo mawili; ukuhani ulihusianishwa pia na makabila hayo, kwa sababu makuhani walitumikia katika hekalu huko Yerusalemu. (2 Nya. 11:13, 14; 34:30) Hivyo, ufalme wa Yuda ulikuwa na wafalme wa ukoo wa Daudi na pia makuhani Walawi. “Kijiti cha Efraimu” kiliwakilisha ufalme wa Israeli wenye makabila kumi. Kijiti hicho kilihusianaje na Efraimu? Mfalme wa kwanza wa ufalme wenye makabila kumi alikuwa Yeroboamu, kutoka kabila la Efraimu. Baadaye, Efraimu likawa kabila kuu katika Israeli. (Kum. 33:17; 1 Fal. 11:26) Ona kwamba ufalme wa Israeli wenye makabila kumi haukuwa na wafalme wa ukoo wa Daudi wala makuhani Walawi.
-
-
Kuunganishwa kwa Vijiti ViwiliHatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 12A
Kuunganishwa kwa Vijiti Viwili
Yehova anamwagiza Ezekieli aandike kwenye kijiti kimoja “kwa ajili ya Yuda” na kingine “kwa ajili ya Yosefu, kijiti cha Efraimu.”
“kwa ajili ya Yuda”
NYAKATI ZA KALE
Ufalme wa Yuda wenye makabila mawili
NYAKATI ZA KISASA
Watiwa mafuta
“kwa ajili ya Yosefu, kijiti cha Efraimu”
NYAKATI ZA KALE
Ufalme wa Israeli wenye makabila kumi
NYAKATI ZA KISASA
Kondoo wengine
-