Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Nitawafanya Kuwa Taifa Moja”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 5. Ni nini maana ya jambo ambalo Ezekieli aliigiza? (Tazama sanduku “Kuunganishwa kwa Vijiti Viwili.”)

      5 Kisha, Yehova akafafanua maana ya kuunganishwa kwa vijiti viwili. (Soma Ezekieli 37:21, 22.) Wahamishwa kutoka ufalme wenye makabila mawili wa Yuda na wahamishwa kutoka ufalme wenye makabila kumi wa Israeli (Efraimu) wangerudi katika nchi ya Israeli, ambako wangekuwa “taifa moja.”—Yer. 30:1-3; 31:2-9; 33:7.

  • “Nitawafanya Kuwa Taifa Moja”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 7. Simulizi lililo kwenye 1 Mambo ya Nyakati 9:2, 3 linathibitishaje kwamba “kwa Mungu mambo yote yanawezekana”?

      7 Kwa maoni ya wanadamu, kukombolewa na kuunganishwa kwa wahamishwa kulionekana kuwa jambo lisilowezekana kabisa.a Hata hivyo, “kwa Mungu mambo yote yanawezekana.” (Mt. 19:26) Yehova alitimiza unabii aliotoa. Utekwa wa Babiloni ulikwisha mwaka wa 537 K.W.K., kisha, watu kutoka falme zote mbili wakafika Yerusalemu ili kurudisha ibada safi. Maandiko yaliyoongozwa na roho yanathibitisha jambo hilo: “Baadhi ya wazao wa Yuda, wa Benjamini, wa Efraimu, na wa Manase [waliishi] Yerusalemu.” (1 Nya. 9:2, 3; Ezra 6:17) Kwa kweli, kama Yehova alivyotabiri, watu kutoka ufalme wenye makabila kumi ya Israeli waliungana na watu kutoka ufalme wa Yuda wenye makabila mawili.

      8. (a) Isaya alitabiri kuhusu nini? (b) Ni mambo gani mawili muhimu yanayopatikana katika Ezekieli 37:21?

      8 Miaka 200 hivi mapema, nabii Isaya alitabiri kuhusu jambo ambalo lingewapata Israeli na Yuda baada ya utekwa. Alitabiri kwamba Yehova angeanza kukusanya pamoja “watu wa Israeli waliotawanywa” nao “watu wa Yuda waliotawanywa [angewakusanya] pamoja kutoka katika pembe nne za dunia,” hata “kutoka Ashuru.” (Isa. 11:12, 13, 16) Na kwa kweli, kama Yehova alivyotabiri, aliwachukua “Waisraeli kutoka katika mataifa.” (Eze. 37:21) Ona mambo mawili muhimu: Kufikia hapa, Yehova hawaiti tena wahamishwa hao “Yuda” na “Efraimu” bali “Waisraeli”—kundi moja. Isitoshe, Waisraeli walifafanuliwa kuwa wanatoka, si katika taifa moja, Babiloni, bali kutoka kwa mataifa mbalimbali, yaani, “kutoka kila upande.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki