Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Niko Dhidi Yako, Ewe Gogu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • Ni “Nchi” Gani Itakayoshambuliwa?

      11. Unabii wa Ezekieli unafafanuaje “nchi” ambayo Gogu ataishambulia?

      11 Kama tulivyozungumzia kwenye fungu la 3, Gogu wa Magogu ataamsha ghadhabu kali ya Yehova kwa kushambulia nchi yenye thamani machoni pa Yehova. Hiyo ni nchi gani? Acheni tuchunguze tena unabii wa Ezekieli. (Soma Ezekieli 38:8-12.) Tunasoma kwamba Gogu ataishambulia “nchi ambayo watu wake wamerudishwa” na kukusanywa “pamoja kutoka katika mataifa.” Ona pia jambo linalosemwa kuhusu waabudu hao waliorudishwa wanaokaa katika nchi hiyo: “Wanakaa kwa usalama”; makazi yao ni “vijiji visivyolindwa na ukuta, makomeo, au malango”; na “wanajikusanyia utajiri.” Hiyo ndiyo nchi ambayo waabudu wa kweli wa Yehova duniani kote wanakaa. Tunawezaje kuitambua?

      12. Ni kurudishwa gani kulikotokea katika nchi ya Israeli nyakati za Biblia?

      12 Inafaa tuchunguze kurudishwa kwa ibada safi katika Israeli la kale, nchi ambamo kwa karne nyingi watu wa Mungu waliochaguliwa waliishi, walifanya kazi, na kuabudu. Waisraeli walipokosa kuwa waaminifu, Yehova alitabiri kupitia Ezekieli kwamba nchi yao ingeharibiwa na kuachwa ukiwa. (Eze. 33:27-29) Lakini Yehova alitabiri pia kwamba watu wachache wangerudi kutoka uhamishoni Babiloni na kurudisha ibada safi katika nchi hiyo. Kupitia baraka za Yehova, nchi ya Israeli ingebadilika, ingesitawi “kama bustani ya Edeni.” (Eze. 36:34-36) Hilo lilitokea kuanzia mwaka wa 537 K.W.K. wahamishwa Wayahudi waliporudi Yerusalemu na kurudisha ibada safi katika nchi yao waliyoipenda.

      13, 14. (a) Nchi ya kiroho ni nini? (b) Kwa nini nchi hiyo ni yenye thamani machoni pa Yehova?

      13 Katika nyakati zetu, waabudu wa kweli wa Mungu waliona kurudishwa kama huko. Kama tulivyojifunza katika Sura ya 9 ya kitabu hiki, mwaka wa 1919, watu wa Mungu walikuwa wamewekwa huru baada ya kuwa utekwani kwa muda mrefu katika Babiloni Mkubwa. Mwaka huo, Yehova aliwaleta waabudu wake waliorudishwa katika nchi ya kiroho. Nchi hiyo ni paradiso ya kiroho—mazingira salama yenye ufanisi wa kiroho, au mahali pa utendaji ambapo tunamwabudu Mungu wa kweli. Tunakaa katika nchi hiyo pamoja kwa usalama, tukiwa na amani ya akilini na moyoni. (Met. 1:33) Tunapokea chakula kingi cha kiroho, na tuna kazi nyingi yenye kuridhisha katika kutangaza Ufalme wa Mungu. Kwa kweli, tunaona ukweli wa methali hii: “Baraka ya Yehova ndiyo inayomtajirisha mtu, naye haichanganyi na maumivu.” (Met. 10:22) Popote tunapoishi duniani, tunakaa katika nchi hiyo—paradiso ya kiroho—maadamu tu tunaunga mkono kwa bidii ibada safi kwa maneno na matendo.

      14 Nchi hii ya kiroho ni yenye thamani machoni pa Yehova. Kwa nini? Machoni pake, wakaaji wake ni “vitu vyenye thamani vya mataifa yote,” watu ambao amewavuta wajiunge na ibada safi. (Hag. 2:7; Yoh. 6:44) Wanajitahidi kuvaa utu mpya, unaopatana na viwango vya juu vya Mungu. (Efe. 4:23, 24; 5:1, 2) Wakiwa waabudu wa kweli, wanajitoa kikamili katika utumishi wake, wakifanya hivyo kwa njia zinazomletea sifa na kuonyesha kwamba wanampenda. (Rom. 12:1, 2; 1 Yoh. 5:3) Tunaweza kuwazia jinsi Yehova anavyopata shangwe nyingi anapoona waabudu wake wakijitahidi kurembesha nchi hiyo ya kiroho. Fikiria jambo hili: Unapotanguliza ibada ya kweli maishani, unarembesha paradiso ya kiroho na pia unafanya moyo wa Yehova ushangilie!—Met. 27:11.

      Mkusanyo wa picha: Waabudu wa Yehova: 1. Ndugu na dada wanafurahia ushirika kwenye Jumba la Ufalme. 2. Ndugu na dada wanasaidiana kudumisha Jumba la Ufalme. 3. Ndugu aliyefungwa gerezani anasali. 4. Mume na mke wanamtembelea dada ambaye ni mgonjwa sana hospitalini.

      Hata iwe tunaishi wapi, tuko katika nchi ya kiroho maadamu tunaunga mkono ibada safi kwa bidii (Tazama fungu la 13 na 14)

  • “Niko Dhidi Yako, Ewe Gogu”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
    • 16 Gogu wa Magogu atashambulia lini nchi yetu ya kiroho iliyorudishwa? Unabii huo unajibu hivi: “Katika miaka ya mwisho utaishambulia nchi [hiyo].” (Eze. 38:8) Hilo linamaanisha kipindi kilicho karibu na mwisho wa mfumo huu wa mambo. Kumbuka kwamba dhiki kuu itaanza na kuharibiwa kwa Babiloni Mkubwa, milki ya ulimwenguni pote ya dini ya uwongo. Baada ya mashirika ya dini ya uwongo kuharibiwa na kabla ya Har–Magedoni kuanza, Gogu atafanya shambulizi kali la mwisho dhidi ya waabudu wa kweli.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki