-
“Jina la Jiji Hilo . . . Litakuwa, Yehova Yupo Hapo”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
4. Tunajifunza somo gani kutokana na simulizi kuhusu mchango kwa Yehova?
4 Tunajifunza somo gani katika simulizi hili kuhusu mchango kwa Yehova? Kwa kutenga kwanza eneo kwa ajili ya mchango wa pekee na kisha maeneo ya makabila, Yehova alionyesha kwamba kituo hicho cha mambo ya kiroho kilipaswa kuwa muhimu zaidi. (Eze. 45:1) Bila shaka, wahamishwa walijifunza mengi kutokana na mpangilio huo wa kugawa nchi. Walipaswa kutanguliza ibada ya Yehova maishani. Vivyo hivyo, leo tunaona mambo ya kiroho, kama vile kujifunza Neno la Mungu, kuhudhuria mikutano ya Kikristo, na kuhubiri, kuwa mambo muhimu zaidi. Tunaiga mfano wa Yehova wa kutanguliza mambo muhimu kwa kufanya ibada yake iwe jambo kuu katika maisha yetu ya kila siku.
-
-
“Mchango Mtakaoweka Kando”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
D. “Mchango Mtakatifu”
Eneo hili linafafanuliwa pia kuwa “sehemu takatifu.” Sehemu ya juu ni kwa ajili ya “Walawi.” Ni “kitu kitakatifu.” Sehemu ya katikati ni “mchango mtakatifu kwa ajili ya makuhani.” Ni “mahali kwa ajili ya nyumba zao, na mahali patakatifu kwa ajili ya patakatifu,” au hekalu.
-