-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
1, 2. Kulingana na Ezekieli 47:1-12, Ezekieli anaona na kujifunza nini? (Tazama picha mwanzoni mwa sura hii.)
EZEKIELI anaona jambo lingine lenye kushangaza katika maono ya hekalu: Kijito kinachotiririka kutoka katika jengo takatifu! Mwazie akichunguza mkondo wa maji hayo yaliyo safi kabisa. (Soma Ezekieli 47:1-12.) Yanatiririka kutoka patakatifu; kisha yanatoka kwenye majengo ya hekalu karibu na lango la mashariki. Malaika anamwongoza Ezekieli kwenda nje ya hekalu, wanapima huku wakienda. Malaika anamwagiza Ezekieli tena na tena apite katika maji, na nabii huyo anatambua kwamba kina cha maji kinaongezeka haraka, na baada ya muda mfupi yanakuwa mengi sana hivi kwamba anaweza tu kuvuka kwa kuogelea!
-
-
“Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
5. Maono ya mto yanaonyeshaje kwamba kutakuwa na baraka za kuwatosha watu wote?
5 Je, sikuzote kungekuwa na baraka za kuwatosha watu wote? Maono hayo yanatoa uhakikisho kwa kuonyesha maji yanayoongezeka kimuujiza—maji kidogo yanayotiririka ambayo baada ya kilomita mbili hivi yanakuwa mengi sana! (Eze. 47:3-5) Huenda idadi ya Wayahudi waliorudishwa ingeongezeka; lakini baraka za Yehova zingeongezeka ili kutosheleza uhitaji huo. Mto huo uliwakilisha maandalizi mengi sana!
-