-
“Jina la Jiji Hilo . . . Litakuwa, Yehova Yupo Hapo”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
“Jiji Litakuwa Katikati Yake”
5, 6. (a) Jiji lilikuwa la nani? (b) Jiji hilo halikuwa nini, na kwa nini?
5 Soma Ezekieli 48:15. “Jiji” na maeneo yaliyolizunguka yalikuwa na maana gani? (Eze. 48:16-18) Yehova alikuwa amemwambia hivi Ezekieli katika maono: “Jiji . . . [litakuwa la] watu wote wa nyumba ya Israeli.” (Eze. 45:6, 7) Basi, jiji na maeneo yaliyolizunguka hayakuwa sehemu ya “mchango mtakatifu” ambao ulipaswa ‘kuwekwa kando kwa ajili ya Yehova.’ (Eze. 48:9) Tukiwa na hilo akilini, acheni tuchunguze jambo tunalojifunza leo kutokana na mpangilio wa jiji hilo.
6 Ili kujifunza masomo kutokana na jiji hilo, kwanza tunahitaji kujua, jiji hilo halikuwa nini? Halikuwa jiji la Yerusalemu pamoja na hekalu lake lililojengwa upya. Kwa nini? Kwa sababu jiji ambalo Ezekieli aliona katika maono halingekuwa na hekalu ndani yake. Pia, jiji hilo halikuwa jiji lingine katika nchi ya Israeli iliyorudishwa. Kwa nini? Kwa maana wahamishwa waliorudi pamoja na wazao wao hawakujenga jiji lenye mambo yaliyotajwa katika maono. Isitoshe, jiji hilo halikuwa jiji la kimbingu. Kwa nini? Kwa kuwa lilijengwa kwenye eneo lililotengwa kwa ajili ya “matumizi ya kawaida [au, matumizi yasiyo matakatifu]” tofauti na majengo yaliyojengwa kwenye eneo lililotengwa hasa kwa ajili ya ibada takatifu.—Eze. 42:20.
7. Jiji ambalo Ezekieli aliona ni nini, na inaelekea linawakilisha nini? (Tazama picha mwanzoni mwa sura hii.)
7 Basi, jiji ambalo Ezekieli aliona ni nini? Kumbuka kwamba aliona jiji hilo katika maono yaleyale aliyoona nchi. (Eze. 40:2; 45:1, 6) Neno la Mungu linaonyesha kwamba nchi hiyo ni nchi ya kiroho, basi jiji hilo linamaanisha jiji la kiroho. Kwa ujumla, neno “jiji” linamaanisha nini? Neno hilo linatoa wazo la watu wanaoishi pamoja katika kikundi na kufanyiza mfumo wenye utaratibu na mpangilio. Basi, inaonekana jiji lenye mpangilio mzuri ambalo Ezekieli aliona—lililokuwa mraba kamili—linawakilisha kituo cha usimamizi chenye mpangilio mzuri.
8. Kituo hicho cha usimamizi kinaongoza milki, au eneo gani, na kwa nini?
8 Kituo hicho cha usimamizi kinaongoza milki, au eneo gani? Maono ya Ezekieli yanafunua kwamba jiji hilo linafanya kazi katika nchi ya kiroho. Basi, leo kituo hicho cha usimamizi kinaongoza katika utendaji wa watu wa Mungu. Wazo la kwamba jiji hilo liko katika eneo la matumizi ya kawaida, au lisilo takatifu linamaanisha nini? Hilo linatukumbusha kwamba jiji hilo si usimamizi wa kimbingu, bali ulio duniani, ambao umekuwa ukitenda kwa faida ya watu wote walio katika paradiso ya kiroho.
-
-
“Mchango Mtakaoweka Kando”Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
-
-
“Eneo Linalobaki”
Litakuwa la “watu wote wa nyumba ya Israeli” na “litakuwa la matumizi ya kawaida ya jiji, kwa ajili ya makao na malisho.”
-