-
Kitabu Cha Biblia Namba 27—Danieli“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
20. Ni njozi gani nne zilizoandikwa kuhusu zile serikali kubwa za ulimwengu, na kwa nini kufikiria njozi hizo leo kwaimarisha imani?
20 Kupitia njozi za Danieli kwasisimua na kuimarisha imani. Kwanza, fikiria zile njozi nne kuhusu serikali kubwa za ulimwengu: (1) Kuna ile njozi juu ya taswira yenye kutia hofu, ambayo kichwa chayo cha dhahabu chawakilisha nasaba ya wafalme wa Kibabuloni kuanzia na Nebukadreza, ambayo baada yayo zainuka falme nyingine tatu, kama zilivyofananishwa na sehemu nyingine za mfano huo. Hizo ndizo falme zinazopondwa na lile “jiwe,” nalo lawa “ufalme ambao hautaangamizwa milele,” Ufalme wa Mungu. (2:31-45) (2) Ndipo zafuata zile njozi za faragha za Danieli, ya kwanza ikiwa ya wale hayawani wanne, wakiwakilisha “wafalme wanne.” Hao wako kama simba, dubu, chui mwenye vichwa vinne, na hayawani mmoja mwenye meno makubwa ya chuma, pembe kumi, na baadaye pembe ndogo moja. (7:1-8, 17-28) (3) Halafu, kuna ile njozi juu ya kondoo ndume (Umedi-Uajemi), yule beberu (Ugiriki), na ile pembe ndogo. (8:1-27) (4) Mwishowe, tuna ile njozi juu ya mfalme wa kusini na mfalme wa kaskazini. Danieli 11:5-19 yasimulia kwa usahihi ushindani uliokuwa kati ya vichipukizi vya Misri na vya Seleucus ambavyo vilitokana na Milki ya Kigiriki ya Aleksanda kufuatia kifo cha Aleksanda katika 323 K.W.K. Kuanzia mstari 20 unabii waendelea kufuatisha mwendo wa mataifa yaliyofuatana ya kusini na kaskazini. Mrejezo wa Yesu kuhusu “chukizo la uharibifu” (11:31), katika unabii wake juu ya ishara ya kuwapo kwake, waonyesha kwamba huku kung’ang’ania mamlaka kwa wale wafalme wawili kwaendelea moja kwa moja mpaka “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mt. 24:3, NW) Uhakikisho ambao unabii huo watoa wafariji kama nini kwamba katika “wakati wa taabu, [ambao] mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa hata wakati uo huo,” Mikaeli mwenyewe atasimama ili kuondoa mataifa yasiyomcha Mungu na kuletea ainabinadamu watiifu amani!—Dan. 11:20–12:1.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 27—Danieli“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
23. (a) Tumaini la Ufalme lakaziwaje katika Danieli yote? (b) Kitabu hiki cha unabii chapasa kututia moyo tufanye nini?
23 Tumaini la Ufalme lakaziwa katika sehemu zote za kitabu cha Danieli kwa njia yenye kutia imani! Yehova Mungu aonyeshwa kuwa ndiye Mwenye Enzi Aliye Mkuu Zaidi anayesimamisha Ufalme ambao hautaangamizwa kamwe na ambao utaponda falme nyingine zote. (2:19-23, 44; 4:25) Hata wafalme wapagani Nebukadreza na Dario walishurutishwa kukiri kwamba Yehova ana ukuu uzidio wa wengine wote. (3:28, 29; 4:2, 3, 37; 6:25-27) Yehova akwezwa na kutukuzwa kuwa Mkale wa Siku anayehukumu lile suala la Ufalme na kumpa “mmoja aliye mfano wa mwanadamu” ile “mamlaka, na utukufu, na ufalme [wa milele], ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie.” “Watakatifu wa Aliye juu” ndio washiriki pamoja na Kristo Yesu, “Mwana wa Adamu,” katika ule Ufalme. (Dan. 7:13, 14, 18, 22; Mt. 24:30; Ufu. 14:14) Yeye ndiye Mikaeli, mwana-mfalme aliye mkuu, ambaye anatumia mamlaka yake ya Ufalme kuponda na kukomesha falme zote za ulimwengu huu mwovu. Kuelewa unabii huo mbalimbali na njozi hizo kwapasa kuwatie moyo wapenda-uadilifu wajitie bidii na kwenda mbio huko na huko katika kurasa za Neno la Mungu ili kupata ‘mambo ya ajabu’ ya makusudi ya Ufalme wa Mungu ambayo twafunuliwa kupitia kitabu cha Danieli kilichopuliziwa na Mungu na chenye mafaa.—Dan. 12:2, 3, 6.
-