-
Imani Yao Ilishinda Jaribu KaliSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
12. Wakaldayo fulani waliwashtaki Waebrania hao watatu juu ya nini, na kwa nini?
12 Kukataa kwa maofisa hao watatu Waebrania kuabudu sanamu hiyo kuliwaghadhibisha Wakaldayo fulani. Mara moja, wakamwendea mfalme “wakaleta mashitaka juu ya Wayahudi.”d Hawakutaka kujua sababu. Wakitaka Waebrania hao wahukumiwe kwa sababu ya kutokuwa waaminifu-washikamanifu na kwa sababu ya uhaini, washtaki hao walisema hivi: “Wako Wayahudi kadha wa kadha uliowaweka juu ya mambo ya wilaya ya Babeli, yaani, Shadraka, na Meshaki, na Abednego; watu hawa, Ee mfalme, hawakukujali wewe; hawaitumikii miungu yako, wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”—Danieli 3:8-12.
-
-
Imani Yao Ilishinda Jaribu KaliSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
d Usemi wa Kiaramu unaotafsiriwa “-leta mashitaka” wamaanisha ‘kula vipande’ vya mtu—kana kwamba kumtafuna kwa kumchongea.
-