-
Aokolewa Asiliwe na Simba!Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
12. (a) Danieli alifanya nini mara tu alipopata kujua juu ya sheria hiyo mpya? (b) Ni nani waliokuwa wakimtazama Danieli, na kwa nini?
12 Upesi Danieli akapata kujua juu ya sheria hiyo iliyokataza kutoa sala. Mara moja, akaingia nyumbani mwake na kwenda kwenye chumba cha paa, ambapo madirisha yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu.b Huko, Danieli akaanza kusali kwa Mungu “kama ilivyokuwa kawaida yake.” (BHN) Huenda Danieli alifikiri alikuwa peke yake, lakini waliompangia njama walikuwa wakimtazama. Ghafula,“waliingia ndani,” yamkini kwa njia ileile walivyokusanyika kwa rabsharabsha walipomwendea Dario. Sasa walikuwa wakiona kwa macho yao wenyewe—Danieli alikuwa “akiomba dua na kumsihi Mungu wake.” (Danieli 6:10, 11, BHN) Mawaziri na maliwali walikuwa na uthibitisho wote waliouhitaji wa kumshtaki Danieli mbele ya mfalme.
-
-
Aokolewa Asiliwe na Simba!Sikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
b Chumba cha paa kilikuwa chumba cha faragha ambacho mtu angeweza kwenda ikiwa hakutaka kusumbuliwa.
-