Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Cha Biblia Namba 27—Danieli
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 6. Ni sehemu gani mbili zinazofanyiza kitabu cha Danieli?

      6 Wayahudi walitia kitabu cha Danieli, si pamoja na Manabii, bali na Maandishi. Kwa upande mwingine, Biblia ya Kiswahili hufuata utaratibu wa orodha ya Septuagint ya Kigiriki na Vulgate ya Kilatini kwa kuweka Danieli kati ya manabii wa umaana mkubwa na mdogo. Kwa kweli kuna sehemu mbili kuhusiana na kitabu hicho. Ya kwanza kati yazo, ambayo ni sura ya 1 hadi ya 6, yafuata utaratibu wa kuorodhesha mfuatano wa matukio wakati inapoonyesha mambo yaliyopata Danieli na waandamani wake katika utumishi wa kiserikali kuanzia 617 K.W.K. hadi 538 K.W.K. (Dan. 1:1, 21) Sehemu ya pili, iliyo na sura ya 7 hadi ya 12, imeandikwa kwa kutumia mtajo wa nafsi ya kwanza, Danieli mwenyewe akiwa ndiye mwenye kuandika, na yasimulia njozi za faragha na mahoji ya kimalaika ambayo Danieli alikuwa nayo kuanzia karibu 553 K.W.K.f hadi karibu 536 K.W.K. (7:2, 28; 8:2; 9:2; 12:5, 7, 8) Sehemu hizo mbili zikiwa pamoja zafanyiza kile kitabu kimoja cha Danieli kilicho na upatani.

  • Kitabu Cha Biblia Namba 27—Danieli
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 7. Ni nini kinachoongoza kwenye mwingio wa Danieli na waandamani wake katika utumishi wa serikali ya Babuloni?

      7 Matayarisho kwa ajili kutumikia Nchi (1:1-21). Katika 617 K.W.K. Danieli aja Babuloni pamoja na Wayahudi watekwa. Vyombo vitakatifu kutoka hekalu la Yerusalemu vyaletwa pia, navyo vyawekwa katika nyumba-hazina ya kipagani. Danieli na waandamani wake watatu Waebrania wamo miongoni mwa vijana Wayudea wa kifalme wanaochaguliwa kwa ajili ya mtaala (mafunzo) wa miaka mitatu wa mazoezi katika jumba la mfalme. Akiwa ameazimia moyoni mwake asijichafue kwa vyakula vitamu-vitamu vya kipagani na divai ya mfalme, Danieli apendekeza mtihani wa siku kumi wa kula mboga. Matokeo ya mtihani huo ni yenye kibali kwa Danieli na waandamani wake, na Mungu awapa maarifa na hekima. Nebukadreza awaweka rasmi hao wanne wasimame mbele yake wakiwa washauri. Mstari wa mwisho sura ya 1, ambao huenda ukawa uliongezwa muda mrefu baada ya kile kisehemu kinachoutangulia kuwa kimeandikwa, waonyesha kwamba Danieli alikuwa angali katika utumishi wa kifalme kwa miaka ipatayo 80 baada ya yeye kwenda uhamishoni, hiyo ingekuwa ni karibu 538 K.W.K.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki