Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wakati wa Kuja Kwa Mesiya Wafunuliwa
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • 25 Ingawa dhambi na kifo viliendelea kuwataabisha wanadamu, kukatiliwa mbali kwa Yesu katika kifo na kufufuliwa kwake na kupata uhai wa kimbingu kulitimiza unabii. “Ku[li]komesha makosa, na kuishiliza dhambi, na kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, na kuleta haki.” Mungu alikuwa ameondoa agano la Sheria, lililokuwa limewafunua na kuwahukumu Wayahudi kuwa watenda-dhambi. (Waroma 5:12, 19, 20; Wagalatia 3:13, 19; Waefeso 2:15; Wakolosai 2:13, 14) Sasa dhambi za watenda-dhambi wenye kutubu zingeweza kufutiliwa mbali, na adhabu yake ingeweza kuondolewa. Kupitia dhabihu yenye kuridhisha ya Mesiya, watu wenye kudhihirisha imani wangeweza kupatanishwa na Mungu. Wangeweza kutazamia kwa hamu kupokea zawadi ya Mungu ya “uhai udumuo milele kwa njia ya Kristo Yesu.”—Waroma 3:21-26; 6:22, 23; 1 Yohana 2:1, 2.

  • Wakati wa Kuja Kwa Mesiya Wafunuliwa
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
    • 27. ‘Ni mahali gani Patakatifu kabisa’ palipotiwa mafuta, na jinsi gani?

      27 Unabii huo ulitabiri pia juu ya kutiwa mafuta kwa “mahali patakatifu kabisa.” Hilo halirejezei kutiwa mafuta kwa Mahali Patakatifu kabisa, au sehemu ya ndani kabisa, ya hekalu la Yerusalemu. Maneno “mahali patakatifu kabisa” hapa yarejezea patakatifu pa kimbingu pa Mungu. Huko, Yesu alimpa Baba yake thamani ya dhabihu yake ya kibinadamu. Ubatizo wa Yesu, mwaka wa 29 W.K., ulitia mafuta, au kutenga, mahali hapo halisi pa kimbingu na pa kiroho palipowakilishwa na Mahali Patakatifu kabisa pa tabenakulo na hekalu la baadaye duniani.—Waebrania 9:11, 12.

      UNABII WATHIBITISHWA NA MUNGU

      28. Ni nini kilichomaanishwa na ‘kutia muhuri maono na nabii’?

      28 Unabii wa Kimesiya uliotolewa na malaika Gabrieli ulisema juu ya “kutia muhuri maono na unabii [“nabii,” NW].” Hilo lamaanisha kwamba kila kitu kilichotabiriwa kuhusu Mesiya—yote ambayo alitimiza kupitia dhabihu yake, kufufuliwa kwake, na kutokea kwake mbinguni, na pia mambo mengine yaliyotukia katika juma la 70—vingetiwa muhuri wa kibali cha Mungu, vingethibitika kuwa kweli, na vingetumainika. Ono hilo lingetiwa muhuri, limhusu Mesiya peke yake. Lingetimizwa kwake yeye na katika kazi ya Mungu kupitia yeye. Tungeweza kupata maana sahihi ya ono hilo kupitia tu Mesiya aliyeahidiwa. Hakuna kitu kingine chochote ambacho kingefunua maana yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki