-
‘Hapana Amani kwa Wabaya’Mnara wa Mlinzi—1987 | Julai 1
-
-
16 Hizi siku za kumalizia hasa ni ngumu kwa watu wa Mungu, ambao katika wakati wa karne hii, wamekuwa wakiteswa na wafalme wote wawili. Yule malaika alionya kwamba mfalme wa kaskazini “ataingia katika hiyo nchi ya uzuri [nchi ya Pambo, NW], na nchi nyingi zitapinduliwa.” Hiyo “nchi ya uzuri [nchi ya Pambo, NW]” kwa usemi wa mfano ni nchi ya watu wa Mungu. Maneno ya malaika lazima yamaanishe, basi, kwamba pamoja na kushinda mataifa mengi, mfalme wa kaskazini anashambulia hali ya kiroho ya watu wa Yehova. (Danieli 8:9; 11:41-44; Ezekieli 20:6) Katika mstari wa 45, unabii unaongeza hivi: “Naye ataweka hema zake za kifalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa uzuri [Pambo].” Kwa maneno mengine, yeye anajiweka katika hali ya kufanya shambulio la mwisho dhidi ya paradiso yao ya kiroho.
-
-
‘Hapana Amani kwa Wabaya’Mnara wa Mlinzi—1987 | Julai 1
-
-
18. (a) Ni nini kilicho chanzo cha zile “ripoti” zilizotabiriwa na yule malaika? (b) Ni nini yatakayokuwa matokeo ya mwisho kwa mfalme wa kaskazini?
18 Ripoti hizo zitakuwa nini? Yule malaika hataji waziwazi, lakini yeye anafunua chanzo chazo. Zinatoka “mashariki,” na Yehova Mungu na Yesu Kristo wanadokezwa kuwa “wafalme wa mashariki.” (Ufunuo 16:12, HNWW) Ripoti hizo pia zinatoka “kaskazini,” na Biblia inasema kwa njia ya mfano kuhusu Mlima Sayuni, ule mji wa Mfalme mkuu Yehova kuwa ukiwa “pande za kaskazini.” (Zaburi 48:2) Kwa sababu hiyo, ni “ripoti” kutoka kwa Yehova Mungu na Yesu Kristo ndizo zinazompeleka mfalme wa kaskazini kwenye kampeni yake kubwa ya mwisho. Lakini matokeo yatakuwa yenye kumharibu. Mwisho wa mstari wa 45 unatuambia hivi: “Lakini atafikilia [mwisho wake, NW], wala hakuna atakayemsaidia.”
-
-
Mikaeli Yule Mwana-Mfalme Mkuu AsimamaMnara wa Mlinzi—1987 | Julai 1
-
-
2, 3. (a) Ni unabii gani ambao tunapata katika kitabu cha Ezekieli unaotusaidia kufahamu unabii juu ya mfalme wa kaskazini na mfalme wa kusini? (b) Kulingana na unabii wa Ezekieli, ni nini yatakayokuwa matokeo ya lile shambulio kuu la mwisho juu ya watu wa Mungu?
2 Unabii uliotolewa na Ezekieli aliyeishi wakati mmoja na Danieli unatusaidia kujibu maswali hayo. Ezekieli, pia, aliongozwa kwa roho aseme juu ya “ile sehemu ya mwisho kabisa ya zile siku,” naye alionya juu ya shambulio linalokuja juu ya ‘Gogu wa Magogu’ dhidi ya nchi ya watu wa Mungu. (Ezekieli 38:2, 14-16, NW; Danieli 10:14) Katika unabii huo, Gogu anamfananisha Shetani, na majeshi yake yanafananisha mawakili wote wa Shetani wa kidunia ambao wangefanya jaribio kali sana la mwisho la kuwafutilia mbali watu wa Mungu. Kwa kuwa shambulio hili, kama lile la mfalme wa kaskazini, linatukia katika ile sehemu ya mwisho kabisa ya zile siku, ni jambo la akili kukata maneno kwamba mfalme wa kaskazini ‘kuweka hema za kifalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa uzuri’ ni katika kuunga mkono shambulio la Gogu. (Danieli 11:40, 45) Je! shambulio hilo litafaulu?
-