-
Yehova Anafunua Mambo Ambayo “Lazima Yatendeke Upesi”Mnara wa Mlinzi—2012 | Juni 15
-
-
9 Kwa muda mrefu watumishi wa Yehova wamekuwa wakijitahidi kuelewa kile ambacho miguu ya sanamu hiyo inafananisha. Andiko la Danieli 2:41 linasema kwamba mchanganyiko wa chuma na udongo ni “ufalme,” mmoja, si falme nyingi. Kwa hiyo, udongo unafananisha vitu fulani katika utawala wa Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani, ambavyo vinaifanya iwe dhaifu zaidi kuliko Milki ya Roma iliyokuwa na nguvu kama chuma ambacho hakijachanganywa na kitu kingine chochote. Udongo unafananisha “uzao wa wanadamu,” au watu wa kawaida. (Dan. 2:43) Katika Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani, watu wameinuka na kudai haki zao kupitia kampeni za kupigania haki za raia, vyama vya wafanyakazi, na harakati za kutafuta uhuru. Watu wa kawaida wanafanya iwe vigumu kwa Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani kutenda kwa nguvu kama za chuma. Pia, maoni ya kisiasa yanayopingana na matokeo ya uchaguzi yanayokaribiana na ambayo hayaonyeshi wazi mshindi yamedhoofisha uwezo wa hata viongozi maarufu, hivi kwamba hawana mamlaka ya kutekeleza sera zao. Danieli alitabiri hivi: “Sehemu moja ya ufalme huo itakuwa yenye nguvu na nyingine itakuwa dhaifu.”—Dan. 2:42; 2 Tim. 3:1-3.
-
-
Yehova Anafunua Mambo Ambayo “Lazima Yatendeke Upesi”Mnara wa Mlinzi—2012 | Juni 15
-
-
11 Je, idadi ya vidole vya miguu vya sanamu hiyo vina maana ya pekee? Fikiria jambo hili: Katika maono mengine, Danieli anataja idadi hususa, kwa mfano, idadi ya pembe zilizo kwenye vichwa vya wanyama mbalimbali. Idadi hizo zina maana. Hata hivyo, anapoeleza kuhusu ile sanamu, Danieli hataji idadi ya vidole vya miguu. Kwa hiyo, inaonekana kwamba idadi hiyo si muhimu sana kama vile ambavyo idadi ya mikono, vidole, miguu, na nyayo za sanamu hiyo si muhimu. Danieli anataja kihususa kwamba vidole vya miguu vingekuwa mchanganyiko wa chuma na udongo. Kutokana na maelezo yake, tunaweza kukata kauli kwamba Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani ndiyo itakayokuwa ikitawala wakati ambapo “jiwe” linalofananisha Ufalme wa Mungu litakapoipiga miguu ya sanamu hiyo.—Dan. 2:45.
-