Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ufalme Umesimamishwa!
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2022 | Julai
    • 10. (a) Muungano wa Uingereza na Marekani unatimizaje kwa usahihi unabii wa Danieli? (b) Tunapaswa kuepuka hatari gani? (Tazama sanduku “Jihadhari na Udongo wa Mfinyanzi!”)

      10 Kwanza, tofauti na serikali kuu za ulimwengu zilizotajwa mwanzoni katika maono hayo, muungano wa Uingereza na Marekani hauwakilishwi na chuma tu kama vile dhahabu au fedha, bali ni mchanganyiko wa chuma na udongo wa mfinyanzi. Udongo wa mfinyanzi unafananisha “uzao wa wanadamu,” au watu wa kawaida. (Dan. 2:43, maelezo ya chini) Kama inavyoonekana wazi leo, maamuzi yao wakati wa uchaguzi, harakati zao za kutetea haki za kiraia, maandamano makubwa, na vyama vyao vya wafanyakazi, hudhoofisha uwezo wa serikali hiyo kuu ya ulimwengu kutekeleza sera zake.

      Jihadhari na Udongo wa Mfinyanzi!

      Nyayo za chuma na udongo kwenye maono ya Danieli kuhusu sanamu kubwa. Kwenye nyayo zake kuna waandamanaji wenye ghasia, askari wenye ngao, viongozi wa ulimwengu wakifanya mkutano, na washiriki wa Umoja wa Mataifa kwenye kongamano lao.

      Katika unabii wa Danieli, udongo wa mfinyanzi kwenye nyayo za ile sanamu kubwa, unafananisha watu wa kawaida. Wana nguvu za kuwashawishi viongozi wa kisiasa na sera zao. (Dan. 2:41-43) Je, hilo linaweza kutusababishia hatari? Ndiyo! Tusipoulinda moyo wetu, tunaweza kulegeza msimamo wetu wa kutounga mkono upande wowote. Kwa mfano, tunaweza kushawishiwa kukubaliana na maoni ya wale wanaotafuta mabadiliko kupitia maandamano au harakati za kisiasa. (Met. 4:23; 24:21, maelezo ya chini) Tunawezaje kuepuka hatari hiyo? Tunapaswa kukumbuka kwamba Shetani ndiye mtawala wa ulimwengu huu. (1 Yoh. 5:19) Na Ufalme wa Mungu ndio tumaini letu pekee.​—Zab. 146:3-5.

  • Ufalme Umesimamishwa!
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2022 | Julai
    • Jihadhari na Udongo wa Mfinyanzi!

      Nyayo za chuma na udongo kwenye maono ya Danieli kuhusu sanamu kubwa. Kwenye nyayo zake kuna waandamanaji wenye ghasia, askari wenye ngao, viongozi wa ulimwengu wakifanya mkutano, na washiriki wa Umoja wa Mataifa kwenye kongamano lao.

      Katika unabii wa Danieli, udongo wa mfinyanzi kwenye nyayo za ile sanamu kubwa, unafananisha watu wa kawaida. Wana nguvu za kuwashawishi viongozi wa kisiasa na sera zao. (Dan. 2:41-43) Je, hilo linaweza kutusababishia hatari? Ndiyo! Tusipoulinda moyo wetu, tunaweza kulegeza msimamo wetu wa kutounga mkono upande wowote. Kwa mfano, tunaweza kushawishiwa kukubaliana na maoni ya wale wanaotafuta mabadiliko kupitia maandamano au harakati za kisiasa. (Met. 4:23; 24:21, maelezo ya chini) Tunawezaje kuepuka hatari hiyo? Tunapaswa kukumbuka kwamba Shetani ndiye mtawala wa ulimwengu huu. (1 Yoh. 5:19) Na Ufalme wa Mungu ndio tumaini letu pekee.​—Zab. 146:3-5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki