-
Yehova Mungu Wetu Ni Mwenye RehemaMnara wa Mlinzi—1989 | Machi 1
-
-
Mrudie Yehova
Hata wale wanaokosa kwa uzito wanaweza kurudia Yehova na kuonyeshwa rehema. (Zaburi 145:8, 9) Hosea alitaja tena utunzaji mwororo ambao Mungu aliwapa Waisraeli. Ingawa taifa hilo liligeuka dhidi ya Yehova, yeye aliahidi kulirudisha, akisema: ‘Nitawakomboa kaburini; nitawaokoa na mauti.’ Samaria (Israeli) ingelazimika kulipa bei kwa uasi. Lakini Waisraeli walihimizwa wamrudie Mungu kwa maneno yanayofaa, ‘sadaka za midomo kana kwamba ni ng’ombe [wachanga, NW].’ Unabii ulimalizia kwa ile fikira yenye kufariji kwamba wenye hekima na waadilifu wanaotembea katika njia nyoofu za Yehova wangeona shangwe juu ya rehema na upendo wake.—13:1-14:9.
-
-
Yehova Mungu Wetu Ni Mwenye RehemaMnara wa Mlinzi—1989 | Machi 1
-
-
○ 13:14—Yehova hangewaachilia Waisraeli wasiotii kwa kuwaponyosha wakati huo kutoka kwenye mamlaka ya Sheoli wala kuwaponesha na kifo. Yeye hangeonyesha masikitikio yoyote, kwa maana wao hawakustahili rehema. Lakini mtume Paulo alionyesha kwamba hatimaye Mungu angemeza kifo milele na kutangua ushindi wacho. Yehova alionyesha nguvu yake ya kufanya hivyo kwa kuinua Yesu Kristo kutoka kwenye kifo na Sheoli, hivyo akitoa uthibitisho kamili kwamba watu walio katika kumbukumbu ya Mungu watafufuliwa na Mwana wake chini ya utawala wa Ufalme.—Yohana 5:28, 29.
-