-
Kitabu Cha Biblia Namba 28—Hosea“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
12. (a) Hosea ajumlisha nini kwa muhtasari katika sura ya 13? (b) Ni mrejesho gani unaoahidiwa?
12 Katika sura ya 13, Hosea ajumlisha kwa muhtasari yote ambayo yametangulia kuhusu ahadi ya mapema ya Israeli na utunzaji mwororo wa Yehova, na pia usahaulifu wa Israeli na taifa hilo kumgeuka Yehova hatimaye. Yehova ajulisha rasmi hivi: “Nimekupa mfalme katika hasira yangu, nikamwondoa katika ghadhabu yangu.” (13:11) Lakini, hata hivyo, kutakuwa na mrejesho: “Nitawakomboa na nguvu za kaburi; nitawaokoa na mauti; ewe mauti, ya wapi mapigo yako? ewe kaburi, ku wapi kuharibu kwako?” (13:14) Hata hivyo, yatakayopata Samaria yenye uasi yatakuwa mabaya kweli kweli.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 28—Hosea“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
15. Waandikaji wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo watumiaje manukuu kutoka kitabu cha Hosea?
15 Marejezo ya unabii wa Hosea na waandikaji wa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ni yenye mafaa sana pia kwa ajili ya ufikirio wetu leo. Kwa kielelezo, Paulo aonyesha matumizi yenye nguvu ya Hosea 13:14 katika kuzungumza juu ya ufufuo: “Ku wapi, ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, ewe mauti, uchungu wako?” (1 Kor. 15:55) Katika kukazia fadhili-zisizostahiliwa za Yehova kama zilivyoonyeshwa kuelekea vyombo vya rehema, Paulo anukuu Hosea 1:10 na 2:23: “Ni kama vile alivyosema katika Hosea, Nitawaita watu wangu wale wasiokuwa watu wangu, na mpenzi wangu yeye asiyekuwa mpenzi wangu. Tena itakuwa mahali pale walipoambiwa, Ninyi si watu wangu, hapo wataitwa wana wa Mungu aliye hai.” (Rum. 9:25, 26) Petro afupiza vifungu vivyo hivyo vya kutoka Hosea kwa kusema: “Ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.”—1 Pet. 2:10.
-