-
Kitabu Cha Biblia Namba 28—Hosea“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
14. Ni utimizo gani mbalimbali ulio sahihi wa unabii wa Hosea unaopasa kuangaliwa?
14 Kitabu cha Hosea chaimarisha imani katika unabii mbalimbali wa Yehova uliopuliziwa na Mungu. Kila jambo alilotabiri Hosea kuhusu Israeli na Yuda lilitimia. Israeli iliachwa na wapenzi wake miongoni mwa mataifa jirani yenye kuabudu sanamu na ikavuna tufani ya uharibifu kutoka kwa Ashuru katika 740 K.W.K. (Hos. 8:7-10; 2 Fal. 15:20; 17:3-6, 18) Hata hivyo, Hosea alikuwa ametabiri kwamba Yehova angeonyesha Yuda rehema na kuikomboa, lakini si kwa uweza wa kijeshi. Hilo lilitimizwa wakati malaika wa Yehova alipochinja 185,000 ya Waashuri wenye kutisha Yerusalemu. (Hos. 1:7; 2 Fal. 19:34, 35) Hata hivyo, Yuda ilitiwa ndani ya hukumu ya Hosea 8:14: “Nitapeleka moto juu ya miji yake, nao utaziteketeza ngome zake,” utabiri ambao ulipata utimizo wa kuogofya wakati Nebukadreza alipofanya ukiwa Yuda na Yerusalemu, 609-607 K.W.K. (Yer. 34:6, 7; 2 Nya. 36:19) Unabii mwingi wa Hosea juu ya mrejesho ulitimizwa wakati Yehova alipokusanya pamoja Yuda na Israeli, nao ‘walikwea kutoka nchi’ ya uhamisho wao katika 537 K.W.K.—Hos. 1:10, 11; 2:14-23; 3:5; 11:8-11; 13:14; 14:1-9; Ezra 2:1, 3:1-3.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 28—Hosea“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
17. (a) Ni nini la lazima kwa wowote wanaojikwaa na kuingia katika uzinzi wa kiroho? (b) Ni ahadi gani ya Ufalme yenye shangwe iliyomo katika Hosea?
17 Kile kielezi cha mke mzinzi kilichoigizwa waziwazi katika maisha ya Hosea mwenyewe chaonyesha kwamba Yehova achukia sana wale wanaompa kisogo na kufuata njia za ibada ya sanamu na ya bandia, hivyo kufanya uzinzi wa kiroho. Wowote ambao wamejikwaa wakaingia kwenye kosa lazima wamrudie Yehova wakiwa na toba ya kweli na kisha ‘watoe ng’ombe za midomo yao.’ (Hos. 14:2; Ebr. 13:15) Wao waweza kuona shangwe pamoja na baki la wana wa Israeli wa kiroho katika utimizo wa ahadi ya Ufalme ya Hosea 3:5: “Baada ya hayo wana wa Israeli watarejea, na kumtafuta BWANA [Yehova, NW], Mungu wao, na Daudi, mfalme wao; nao watamwendea BWANA [Yehova, NW] na wema wake kwa kicho siku za mwisho.”
-