-
Kitabu Cha Biblia Namba 28—Hosea“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
7. Ni nini kinachotolewa kielezi katika kutoaminika kwa Gomeri na kurudia kwake hali nzuri baadaye?
7 Kwenye mwanzo wa kazi-maisha yake ya kiunabii, Hosea aliamriwa akatwae “mke wa uzinzi.” (1:2) Kwa uhakika Yehova alikuwa na kusudi fulani katika jambo hilo. Israeli walikuwa wamekuwa kwa Yehova kama mke ambaye alikuwa amekuja kuwa asiyeaminika, mwenye kufanya uasherati. Hata hivyo yeye angeonyesha upendo wake kwa mke huyo na kujaribu kumrejesha. Gomeri, mke wa Hosea, angeweza kutoa kielezi sahihi juu ya jambo hilo. Yaeleweka kwamba baada ya kuzaliwa kwa mtoto wa kwanza, alikuja kuwa asiyeaminika na yaonekana kuwa alizaa watoto wale wengine katika uzinzi. (2:5-7) Hiyo yaonyeshwa na taarifa ya maandishi hayo kwamba mke huyo “akamzalia [Hosea] mtoto mwanamume” lakini bila kurejezea nabii huyo inapotaja juu ya kuzaliwa kwa watoto wale wengine wawili. (1:3, 6, 8) Sura ya 3, mistari 1-3, yaelekea kuwa yamnena Hosea kuwa akirejesha Gomeri, akimnunua kama kwamba ni mtumwa, na jambo hilo lahusiana vizuri na Yehova kurejesha watu wake baada ya wao kutubu kutoka kwenye mwendo wao wa uzinzi.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 28—Hosea“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
9. Majina ya watoto wa Gomeri yaonyesha nini juu ya jinsi Yehova angeshughulika pamoja na Israeli?
9 Mwendo wa uzinzi wa Israeli wafanyiwa kielezi (1:1–3:5). “Mke wa uzinzi” wa Hosea amzalia nabii huyo mwana, Yezreeli. Baadaye mke huyo apata watoto wengine wawili, binti, Lo-ruhama, ikimaanisha “[Yeye] Hakuonyeshwa Rehema,” na mwana, Lo-ami, ikimaanisha “Si Watu Wangu.” Yehova aliwapa majina hayo mawili kuonyesha kwamba yeye ‘hangerehemu nyumba ya Israeli tena’ na ili kukazia kuwakataa wao kwa ujumla wasiwe watu wake. (1:2, 6, 9) Hata hivyo, wana wa Yuda na Israeli, wakiwa “wana wa Mungu aliye hai,” watakusanywa katika muungamano chini ya kichwa kimoja, “kwa maana siku ya Yezreeli itakuwa kuu sana.” (1:10, 11) Kwa kuondoshewa ibada ya Baali iliyo ya uzinzi, watu wa Mungu watamrudia Yehova na kumkubali yeye kuwa mume wao. (2:16) Yehova atawapa Israeli usalama na kuwaposa kwake kwa wakati usiojulikana katika uadilifu, katika haki, katika fadhili za upendo, katika rehema nyingi, na katika uaminifu. Kwa kupatana na jina Yezreeli (ambalo lamaanisha “Mungu Atapanda Mbegu”), Yehova aahidi hivi: “Nami nitampanda [kama mbegu, NW] katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; . . . nami nitawaambia wale wasiokuwa watu wangu, Ninyi ndinyi watu wangu; nao watasema, Wewe ndiwe Mungu wangu.” (2:23) Kama mke mwenye kutubu kutoka uzinzi wake, “Israeli watarejea, na kumtafuta BWANA [Yehova, NW], Mungu wao, na Daudi, mfalme wao.”—3:5.
-