Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Cha Biblia Namba 32—Yona
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 4. Yawezekana ni samaki wa aina gani alimmeza Yona? Hata hivyo, ni nini iliyo habari ya kutosha kuturidhisha?

      4 Namna gani juu ya “samaki mkubwa” aliyemeza Yona? Kumekuwako kukisia-kisia kwingi juu ya huyo alikuwa samaki wa aina gani. Nyangumi-shahawa aweza kabisa kumeza binadamu mzima. Ndivyo na yule papa-mweupe mkubwa sana. Hata hivyo, Biblia yaeleza hivi kwa wepesi: “BWANA [Yehova, NW] akaweka tayari samaki mkubwa ili ammeze Yona.” (Yona 1:17) Aina ya samaki huyo haikutajwa. Haiwezi kupambanuliwa kwa uhakika kama alikuwa nyangumi-shahawa, papa-mweupe mkubwa sana, au kiumbe mwingine wa baharini asiyetambulishwa.a Maandishi ya Biblia kwamba alikuwa “samaki mkubwa” ni habari ya kutosha kuturidhisha.

  • Kitabu Cha Biblia Namba 32—Yona
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 6. Yona apatwa na nini kuhusiana na yule “samaki mkubwa”?

      6 Amezwa na “samaki mkubwa” (1:17–2:10). “BWANA [Yehova, NW] akaweka tayari samaki mkubwa ili ammeze Yona, naye Yona akawa ndani ya tumbo la samaki yule muda wa siku tatu, mchana na usiku.” (1:17) Yeye apelekea Yehova sala ya bidii nyingi sana akiwa ndani ya samaki yule. “Akiwa ndani ya tumbo la Sheoli” alilia msaada na kutangaza kwamba atalipa kile ambacho amenadhiri, kwa maana “wokovu ni wa Yehova.” (2:2, 9, NW) Kwa amri ya Yehova, samaki yule amtapika Yona kwenye nchi kavu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki