-
Alijifunza Kuwa Mwenye RehemaIgeni Imani Yao
-
-
8 Mfalme pia alitubu aliposikia ujumbe wa Yona. Aliinuka kutoka kwenye kiti chake cha ufalme, akavua mavazi yake ya kifahari, akavaa nguo za magunia ambazo watu wake walikuwa wamevaa, na hata ‘akaketi katika majivu.’ Akiwa pamoja na “wakubwa” au wakuu, mfalme alitoa agizo rasmi la kufunga, ingawa tayari watu walikuwa wameanza kufunga. Aliamuru watu wote, kutia ndani wanyama wa kufugwa wavae nguo za magunia.b Kwa unyenyekevu, alikiri watu wake walikuwa na hatia ya kutenda mabaya na jeuri. Akionyesha kwamba alitumaini Mungu wa kweli angewaonyesha rehema kwa vile walitubu, mfalme alisema: ‘Huenda Mungu wa kweli atageuka na kuacha hasira yake inayowaka, tusije tukaangamia.’—Yona 3:6-9.
-
-
Alijifunza Kuwa Mwenye RehemaIgeni Imani Yao
-
-
b Huenda hilo likashangaza, lakini lilikuwa jambo la kawaida zamani. Mwanahistoria Mgiriki Herodoto alisema kwamba Waajemi wa kale waliomboleza kifo cha jenerali maarufu kwa kuhusisha wanyama wa kufugwa katika desturi za kuomboleza.
-