-
Kitabu Cha Biblia Namba 33—Mika“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
14. (a) Kisehemu cha 3 cha Mika chaanza kwa kutumia kielezi gani? (b) Ni matakwa gani ya Yehova ambayo watu wa Israeli wameshindwa kutimiza?
14 Sehemu 3 (6:1–7:20). Sasa tamasha ya mahakamani iliyo ya kustaajabisha yatokezwa kwa mtungo wa kimaongezi. Yehova ana “mateto” pamoja na Israeli, naye aita vilima na milima yenyewe iwe mashahidi. (6:1) Atokezea Israeli mwito wa ushindani ili watoe ushuhuda juu yake, naye asimulia vitendo vyake vya uadilifu ambavyo amewafanyia. Yehova ataka nini kwa mwanadamu wa duniani? Si umati wa dhabihu za wanyama, bali “kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu [wake]!” (6:8) Jambo hilo hasa ndilo limekosekana katika Israeli. Badala ya haki na rehema kuna “mizani ya udhalimu,” jeuri, udanganyifu, na vitendo vya hila. (6:11) Badala ya kutembea kwa njia ya kiasi pamoja na Mungu, wao watembea katika mashauri mabovu na ibada ya sanamu ya Omri na Ahabu, waliotawala katika Samaria.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 33—Mika“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
16. (a) Unabii wa Mika ulithibitikaje kuwa wenye mafaa katika siku ya Hezekia? (b) Kina maonyo gani ya upole yaliyo na nguvu kwa ajili ya siku hii ya kisasa?
16 Karibu miaka 2,700 iliyopita, kutoa unabii kwa Mika kulithibitika kuwa kwenye ‘kufaa kuwaonya watu makosa,’ kwa maana Mfalme Hezekia wa Yuda aliitikia ujumbe huo na kuongoza taifa hilo kwenye toba na rekebisho la kidini. (Mika 3:9-12; Yer. 26:18, 19; linganisha 2 Wafalme 18:1-4.) Leo unabii huo uliopuliziwa na Mungu ni wenye mafaa hata zaidi. Sikieni, wote wanaodai kuabudu Mungu, maonyo yaliyo wazi ya Mika juu ya dini bandia, ibada ya sanamu, kusema uwongo, na jeuri! (Mika 1:2; 3:1; 6:1) Paulo arudia maonyo hayo kwenye 1 Wakorintho 6:9-11, ambapo asema kwamba Wakristo wa kweli wamesafishwa wakawa safi na kwamba hakuna yeyote anayejiingiza katika mazoea hayo atakayerithi Ufalme wa Mungu. Kwa wepesi na uwazi, Mika 6:8 yaeleza kwamba takwa la Yehova ni kwa binadamu atembee pamoja Naye katika haki, fadhili, na kiasi.
-