-
Kuwatendea Wengine Kama Mungu AnavyotakaIzingatie Siku ya Yehova Maishani
-
-
6. Tofauti na Zekaria 7:10, andiko la Mika 7:18 linapendekeza tufanye nini?
6 Yehova alimwongoza Zekaria kusema kwamba hataki ‘tupangiane jambo lolote baya mioyoni mwetu.’ (Zekaria 7:9, 10; 8:17) Shauri hilo linafaa hasa tunapohisi kwamba ndugu ametuumiza au amemkosea mtu fulani katika familia yetu. Katika hali kama hizo, ni rahisi ‘kupangiana jambo baya mioyoni mwetu’ na kuonyesha hivyo kwa matendo. Kwa upande mwingine, Mungu anataka tuige mfano wake mzuri. Kumbuka, Mika aliandika kwamba Yehova ‘anasamehe kosa na kuuachilia ukosaji.’a (Mika 7:18) Tutafanyaje hivyo katika shughuli zetu?
7. Kwa nini tunaweza kuamua kuacha tu makosa tuliyotendewa?
7 Huenda tukaumia moyoni kwa sababu ya jinsi tulivyotendewa au jinsi mtu wetu wa ukoo alivyotendewa, lakini kwa kweli, ni jambo zito kadiri gani? Biblia hutaja hatua za kuchukua tunapokosana, au hata tunapomkosea ndugu. Hata hivyo, mara nyingi ni vizuri kutotilia maanani makosa hayo, au ‘kuuachilia ukosaji.’ Jiulize: ‘Je, hii yaweza kuwa moja kati ya zile mara 77 ambazo ninapaswa kumsamehe? Mbona nisiliache tu kosa hilo?’ (Mathayo 18:15-17, 21, 22) Hata ikiwa kosa linaonekana kuwa kubwa sasa, je, litabaki kubwa miaka 1,000 ijayo? Jifunze jambo muhimu kutokana na maelezo ya Mhubiri 5:20 kuhusu mfanyakazi anayefurahia chakula na kinywaji: “Si mara nyingi atakumbuka siku za maisha yake, kwa maana Mungu wa kweli anamshughulisha kwa shangwe ya moyo wake.” Mtu huyo anapofurahia raha yake ya sasa, husahau matatizo anayokabili katika maisha yake ya kila siku. Je, tunaweza kuiga mtazamo huo? Tukikazia fikira shangwe za undugu wetu wa Kikristo, tunaweza kusahau mambo ambayo ni ya muda tu, yale ambayo hatutakumbuka katika ulimwengu mpya. Kufanya hivyo ni tofauti kabisa na kushangilia wengine wanapokabili matatizo au kukumbuka makosa tuliyotendewa.
Mtu anapokukosea, unapaswa kuepuka kufanya nini?
-
-
Kuwatendea Wengine Kama Mungu AnavyotakaIzingatie Siku ya Yehova Maishani
-
-
a Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “kuuachilia ukosaji” kihalisi linamaanisha “kupita kosa.” Kuhusu maneno “kupita kosa,” msomi mmoja anasema kwamba “yanatokana na wazo la msafiri anayepita bila kuona kitu fulani ambacho hataki kukikazia fikira. Haimaanishi [kwamba Mungu haoni dhambi] bali kwamba hakazii uangalifu visa fulani vya dhambi akiwa na nia ya kuadhibu; yeye husamehe badala ya kuadhibu.”
-