-
Watumishi wa Yehova Wana Tumaini la KweliMnara wa Mlinzi—2003 | Agosti 15
-
-
19, 20. Nini kilichotukia kwa Wayahudi waliomtumaini Yehova?
19 Hata hivyo, wale wanaomtumaini Yehova hawatakatishwa tamaa. Yehova ni mwaminifu kwa maagano yake pamoja na Abrahamu na Daudi, naye huwahurumia watu ambao, kama Mika, wanampenda na kuhuzunikia raia wenzao waliotengwa na Mungu. Kwa ajili ya wanyoofu, kutakuwa na urudisho katika wakati wa Mungu unaofaa.
20 Jambo hilo linatukia mwaka wa 537 K.W.K, wakati mabaki ya Wayahudi wanaporudishwa katika nchi yao baada ya Babiloni kuanguka. Wakati huo maneno ya Mika 2:12 yanapata utimizo wa kwanza. Yehova anasema: “Hakika nitakukusanya, Ee Yakobo, nyote pia; bila shaka nitawakusanya waliobaki wa Israeli; nitawaweka pamoja kama kondoo wa Bozra; kama kundi la kondoo kati ya malisho yao; watafanya mvumo kwa wingi wa watu.” Yehova ana upendo ulioje! Baada ya kuwaadhibu watu wake, anaruhusu mabaki warudi na kumtumikia katika nchi aliyowapa babu zao.
-
-
Watumishi wa Yehova Wana Tumaini la KweliMnara wa Mlinzi—2003 | Agosti 15
-
-
22. Ni vikundi gani viwili ambavyo vimeweka tumaini lao katika Ufalme wa Mungu?
22 Katika mwaka wa 1919, Wakristo watiwa-mafuta walio waaminifu walijitenga kabisa na dini zinazodai kuwa za Kikristo nao wakaanza kutangaza habari njema ya Ufalme kwa mataifa yote. (Mathayo 24:14) Kwanza walitafuta waliobaki kati ya Israeli wa kiroho. Kisha wakaanza kukusanya “kondoo wengine,” na vikundi hivyo viwili vikawa “kundi moja, mchungaji mmoja.” (Yohana 10:16) Ingawa sasa wanamtumikia Mungu katika nchi 234, kwa kweli waabudu hao wote waaminifu ‘wamewekwa pamoja.’ Kufikia sasa, kundi la kondoo ‘linavuma kwa wingi wa watu,’ kutia ndani wanawake na watoto. Hawaweki tumaini lao katika mfumo huu wa mambo, bali katika Ufalme wa Mungu, ambao hivi karibuni utaleta paradiso duniani.
-