-
Kitabu cha Biblia Namba 34—Nahumu“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
8. Ni hukumu gani ya maangamizi inayotangaziwa Ninawi, lakini kwa Yuda ni habari gani njema?
8 Tangazo la Yehova juu ya Ninawi (1:1-15). “BWANA [Yehova, NW] ni Mungu mwenye wivu [mwenye kutoza ibada isiyotia ndani wengine, NW], naye hujilipiza kisasi.” Kwa maneno hayo nabii atokeza tamasha kwa ajili ya “ufunuo juu ya Ninawi.” (1:1, 2) Ingawa Yehova ni mpole wa kasirani, mwone sasa akionyesha kisasi kwa kutumia upepo na tufani. Milima yatikisika, vilima vyayeyuka, na dunia yainuka-inuka. Ni nani awezaye kusimama mbele ya joto la kasirani yake? Hata hivyo, Yehova ni ngome kwa ajili ya wale wanaotafuta kimbilio katika yeye. Lakini Ninawi limehukumiwa maangamizi. Litafutiliwa mbali kwa furiko, na “mateso hayatainuka mara ya pili.” (1:9) Yehova atafuta jina lalo na miungu yalo. Yeye atalizika. Kwa utofautisho wenye kuburudisha, zipo habari njema kwa Yuda! Ni nini hizo? Mhubiri wa amani awaita waadhimishe sikukuu zao na kulipa nadhiri zao, kwa maana adui, “yule asiyefaa kitu,” amehukumiwa maangamizi. “Amekwisha kukatiliwa mbali.”—1:15.
-
-
Kitabu cha Biblia Namba 34—Nahumu“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
12. Ni mrejesho gani anaotangaza Nahumu, na unabii wake waweza kukamatanishwaje na tumaini la Ufalme?
12 Kinyume cha Ninawi ‘kukatiliwa mbali,’ Nahumu ajulisha rasmi mrejesho wa ‘fahari ya Yakobo na ya Israeli.’ Pia Yehova apeleka habari za furaha kwa watu wake: “Tazama, juu ya milima iko miguu yake aletaye habari njema, atangazaye amani.” Habari hizo za amani zina uhusiano fulani na Ufalme wa Mungu. Twajuaje hilo? Ni wazi kwa sababu ya matumizi ya Isaya ya usemi uo huo, lakini akiuongezea maneno haya: “Aletaye habari njema ya mambo mema, yeye autangazaye wokovu, auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki!” (Nah. 1:15; 2:2; Isa. 52:7) Kisha, mtume Paulo katika Warumi 10:15 atumia usemi huo kwa wale ambao Yehova awatuma wakiwa wahubiri Wakristo wa habari njema. Wao hupiga mbiu juu ya “habari njema ya ufalme.” (Mt. 24:14) Kwa uhalisi wa maana ya jina lake, Nahumu atoa faraja kwa wote wanaotafuta amani na wokovu unaoambatana na Ufalme wa Mungu. Wote hao watajua kwa uhakika kwamba ‘Yehova ni mwema, ni ngome siku ya taabu kwa wale wamkimbiliao.’—Nah. 1:7.
-