-
Waovu Wataendelea Hata Lini?Mnara wa Mlinzi—2000 | Februari 1
-
-
9 Habakuki asikiliza kwa makini maneno ya Mungu yanayofuata, yaliyorekodiwa kwenye Habakuki 1:6-11. Huu ni ujumbe wa Yehova—wala hakuna mungu asiye wa kweli wala sanamu isiyo na uhai iwezayo kuuzuia usitimizwe: “Kwa maana, angalieni, nawaondokesha Wakaldayo, taifa lile kali, lenye haraka kupita kiasi; wapitao katikati ya dunia, ili wayamiliki makao yasiyo yao. Hao ni watu wa kutisha sana, wa kuogofya sana; hukumu yao na ukuu wao hutoka katika nafsi zao wenyewe. Farasi zao ni wepesi kuliko chui, ni wakali kuliko mbwa-mwitu wa jioni; na wapanda farasi wao hujitapa naam, wapanda farasi wao watoka mbali sana; huruka kama tai afanyaye haraka ale. Waja wote ili kufanya udhalimu; nyuso zao zimeelekezwa kwa bidii yao kama upepo wa mashariki, nao hukusanya mateka kama mchanga. Naam, huwadhihaki wafalme, na wakuu ni kitu cha kudharauliwa kwake; huidharau kila ngome; kwa maana hufanya chungu ya mavumbi, na kuitwaa. Kisha atapita kwa kasi, kama upepo, atapita na kuwa ana hatia; yeye ambaye nguvu zake ni mungu wake.”
-
-
Waovu Wataendelea Hata Lini?Mnara wa Mlinzi—2000 | Februari 1
-
-
11. Ungefafanuaje kuja kwa majeshi ya Babiloni dhidi ya Yuda?
11 Farasi za Babiloni ni wepesi kuliko chui wenye kasi. Jeshi lake la wapanda-farasi ni kali kuliko mbwa-mwitu wenye njaa wawindao usiku. Likiwa na hamu kubwa ya kwenda, ‘huitapa ardhi’ kwa kukosa subira. Tokea Babiloni lililo mbali waelekea Yuda. Hivi karibuni Wakaldayo watayavamia mawindo yao, wakiruka kama tai afanyaye haraka akale mlo mtamu. Je, huo ni uvamizi tu, uporaji ufanywao na askari wachache tu? La! “Waja wote ili kufanya udhalimu,” kama vile jeshi kubwa mno likusanyikavyo ili kuharibu. Nyuso zao zikiwa zimeelekezwa kwa bidii, wapanda-farasi waelekea Yuda na Yerusalemu, wakisonga kasi kama upepo wa mashariki. Majeshi ya Babiloni yateka wafungwa wengi hivi kwamba ni kana kwamba ‘wanakusanya mateka kama mchanga.’
-