-
Waovu Wataendelea Hata Lini?Mnara wa Mlinzi—2000 | Februari 1
-
-
9 Habakuki asikiliza kwa makini maneno ya Mungu yanayofuata, yaliyorekodiwa kwenye Habakuki 1:6-11. Huu ni ujumbe wa Yehova—wala hakuna mungu asiye wa kweli wala sanamu isiyo na uhai iwezayo kuuzuia usitimizwe: “Kwa maana, angalieni, nawaondokesha Wakaldayo, taifa lile kali, lenye haraka kupita kiasi; wapitao katikati ya dunia, ili wayamiliki makao yasiyo yao. Hao ni watu wa kutisha sana, wa kuogofya sana; hukumu yao na ukuu wao hutoka katika nafsi zao wenyewe. Farasi zao ni wepesi kuliko chui, ni wakali kuliko mbwa-mwitu wa jioni; na wapanda farasi wao hujitapa naam, wapanda farasi wao watoka mbali sana; huruka kama tai afanyaye haraka ale. Waja wote ili kufanya udhalimu; nyuso zao zimeelekezwa kwa bidii yao kama upepo wa mashariki, nao hukusanya mateka kama mchanga. Naam, huwadhihaki wafalme, na wakuu ni kitu cha kudharauliwa kwake; huidharau kila ngome; kwa maana hufanya chungu ya mavumbi, na kuitwaa. Kisha atapita kwa kasi, kama upepo, atapita na kuwa ana hatia; yeye ambaye nguvu zake ni mungu wake.”
-
-
Waovu Wataendelea Hata Lini?Mnara wa Mlinzi—2000 | Februari 1
-
-
12. Wababiloni wana mtazamo gani, na adui huyo mwenye nguvu sana ‘anakuwa na hatia’ ya nini?
12 Jeshi la Wakaldayo lawacheka wafalme na kuwadhihaki maofisa wakuu, ambao wote hawana nguvu za kukomesha mashambulizi yake makali. “Huidharau kila ngome,” kwa kuwa ngome yoyote ile huanguka Wababiloni ‘wafanyapo chungu ya mavumbi’ na kuishambulia toka hapo. Wakati uliowekwa rasmi wa Yehova ufikapo, adui huyo mwenye kutisha ‘atapita kwa kasi kama upepo.’ Katika kushambulia Yuda na Yerusalemu, ‘atakuwa na hatia’ ya kuwadhuru watu wa Mungu. Baada ya ushindi wa kasi, kamanda Mkaldayo atajivuna hivi: ‘Nguvu zetu ni mungu wetu.’ Lakini amekosea kama nini!
-