-
Kitabu Cha Biblia Namba 35—Habakuki“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
7. Yehova afarijije Habakuki?
7 Njozi ya ole tano (2:2-20). Yehova ajibu hivi: “Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao.” Hata ikionekana kana kwamba yakawia, itakuwa kweli pasipo shaka. Yehova afariji Habakuki kwa maneno haya: “Lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake.” (2:2, 4) Adui mwenye kujitanguliza hatafikia mradi wake, hata kama aendelea kujikusanyia mataifa na vikundi vya watu. Kwani, ao hao ndio wataanza kusema juu yake ule usemi wa kimithali juu ya zile ole tano:
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 35—Habakuki“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
12. Ni matumizi gani yenye mafaa ya Habakuki 2:4 aliyofanya Paulo?
12 Akitambua unabii wa Habakuki kuwa wenye mafaa kwa kufundisha, mtume Paulo alinukuu kutoka sura ya 2, mstari wa 4, kwenye pindi tatu tofauti. Alipokuwa akikazia kwamba habari njema ni uwezo wa Mungu wa wokovu kwa kila mtu mwenye imani, Paulo aliandikia hivi Wakristo katika Rumi: “Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani.” Alipokuwa akiandikia Wagalatia, Paulo alikazia wazo la kwamba baraka huja kupitia imani: “Kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani.” Alipokuwa akiwaandikia Wagalatia, Paulo alikazia wazo la kwamba baraka huja kupitia imani: “Hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani.” Pia Paulo aliandika katika barua yake kwa Waebrania kwamba Wakristo wapaswa kuonyesha imani iliyo hai, ya kuhifadhi nafsi, na tena yeye alirejezea maneno ya Yehova kwa Habakuki. Hata hivyo, hanukuu maneno ya Habakuki tu, “mwenye haki wangu ataishi kwa imani,” bali pia maneno yake yanayoendelea kwa kulingana na Septuagint ya Kigiriki: “Akisita, nafsi yangu haina upendezi katika yeye.” Kisha ajumlisha kwa muhtasari kwa kusema: Sisi “hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho [nafsi, NW] zetu.”—Rum. 1:17; Gal. 3:11; Ebr. 10:38, 39.
-