Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mtumaini Yehova Uishi
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Novemba
    • 15, 16. (a) Ni ahadi gani zenye kugusa moyo zilizo kwenye kitabu cha Habakuki? (b) Tunajifunza nini kutokana na ahadi hizo?

      15 Yehova anawaahidi hivi watu waadilifu wanaomtumaini: “Mwadilifu ataishi kwa uaminifu wake,” na “dunia itajaa ujuzi wa utukufu wa Yehova.” (Hab. 2:4, 14) Naam, wale wote wanaoendelea kumtumaini Mungu kwa subira watathawabishwa kwa kupewa uzima.

  • Mtumaini Yehova Uishi
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Novemba
    • 17. Kitabu cha Habakuki kinatuhakikishia nini?

      17 Kitabu cha Habakuki kinatufundisha somo muhimu sana sisi tunaoishi katika siku hizi za mwisho. Yehova anaahidi kumpa uzima mtu yeyote mwadilifu anayemwamini na kumtumaini. Acheni tuendelee kuimarisha imani yetu kwa Mungu na kuendelea kumtumaini, hata iwe tunakabili matatizo au mikazo gani maishani. Kupitia nabii Habakuki, Yehova anatuhakikishia kwamba atatutegemeza na kutuokoa. Kwa fadhili, anatusihi tumtumaini na kungojea kwa subira wakati wake uliowekwa, ambapo chini ya Ufalme wake dunia nzima itajawa na waabudu wake wenye furaha na wenye sifa ya upole.—Mt. 5:5; Ebr. 10:36-39.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki