-
“Mikono Yako Isilegee”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
11, 12. (a) Ni sehemu ipi nyingine ya unabii wa Sefania ambayo imetimizwa juu ya mabaki? (b) Mabaki watiwa-mafuta wametiije mwito huu, “Mikono yako isilegee”?
11 Mabaki waaminifu hushangilia kwa kukombolewa katika 1919 kutoka utekwa wa kiroho wa Babiloni Mkubwa, milki ya ulimwengu ya dini bandia. Wao wameona utimizo wa unabii wa Sefania: “Imba, Ee binti Sayuni; piga kelele, Ee Israeli; furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, Ee binti Yerusalemu. BWANA ameziondoa hukumu zako, amemtupa nje adui yako; mfalme wa Israeli, naam, yeye BWANA, yu katikati yako; hutaogopa uovu tena. Katika siku ile Yerusalemu utaambiwa, usiogope, Ee Sayuni; mikono yako isilegee. BWANA, Mungu wako, yu katikati yako shujaa awezaye kuokoa.”—Sefania 3:14-17.
12 Kwa usadikisho wenye nguvu na uthibitisho mwingi sana kwamba Yehova yuko katikati yao, mabaki watiwa-mafuta wamesonga mbele bila kuogopa ili kutimiza utume wao wa kimungu. Wao wamehubiri habari njema ya Ufalme nao wamejulisha hukumu za Yehova dhidi ya Jumuiya ya Wakristo, sehemu nyingine ya Babiloni Mkubwa, na mfumo wote mwovu wa Shetani. Japo magumu yote, kwa miongo mingi tangu 1919, wao wametii amri hii ya kimungu: “Usiogope, Ee Sayuni; mikono yako isilegee.” Wao wamekuwa na bidii katika kugawanya mabilioni ya trakti, magazeti, vitabu, na vijitabu vyenye kutangaza Ufalme wa Yehova. Hao wamekuwa vielelezo vyenye kuimarisha imani kwa kondoo wengine ambao wamewaunga mkono kwa wingi tangu 1935.
-
-
“Mikono Yako Isilegee”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
16. Ni hali gani ya akili iliyo miongoni mwa washiriki wengi wa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo, lakini Yehova atupa kitia-moyo gani?
16 Kutojali ndiko mtazamo wenye kuenea leo katika sehemu nyingi za dunia, hasa katika nchi zilizo tajiri zaidi. Hata washiriki wa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo hawaamini kamwe kwamba Yehova Mungu ataingilia mambo ya kibinadamu katika siku yetu. Wao hupuuza jitihada zetu za kuwafikia kwa habari njema za Ufalme kwa tabasamu yenye kutilia shaka au kwa jibu fupi “Sipendezwi!” Chini ya hali hizo, udumifu katika kazi ya kutoa ushahidi waweza kuwa mgumu sana. Hilo hujaribu uvumilivu wetu. Lakini kupitia unabii wa Sefania, Yehova huwachochea watu wake waaminifu, akisema: “Mikono yako isilegee. BWANA, Mungu wako, yu katikati yako shujaa awezaye kuokoa; atakushangilia kwa furaha kuu, atakutuliza katika upendo wake, atakufurahia kwa kuimba.”—Sefania 3:16, 17.
17. Ni kielelezo kipi kizuri ambacho wapya miongoni mwa kondoo wengine wapaswa kufuata, na jinsi gani?
17 Ni jambo la hakika katika historia ya kisasa ya watu wa Yehova kwamba mabaki, na vilevile wale walio wazee-wazee zaidi miongoni mwa kondoo wengine, wametimiza kazi kubwa sana ya ukusanyaji katika hizi siku za mwisho. Wakristo hawa wote waaminifu wameonyesha uvumilivu katika miongo ambayo imepita. Wao hawajaruhusu kutojali kwa upande wa wengi katika Jumuiya ya Wakristo kuwavunje moyo. Basi, na wale walio wapya miongoni mwa kondoo wengine na wasijiachilie wavunjwe moyo na hali ya kutojali mambo ya kiroho ambayo imeenea sana leo katika nchi nyingi. Na wasiache ‘mikono yao ilegee,’ au kukosa bidii. Na watumie kila fursa wapatayo kutoa Mnara wa Mlinzi, Amkeni!, na vichapo vingine vizuri vilivyokusudiwa kusaidia watu wenye mfano wa kondoo kujifunza kweli kuhusu siku ya Yehova na baraka zitakazofuata.
-
-
“Mikono Yako Isilegee”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
18, 19. (a) Ni kitia-moyo gani cha kuvumilia tupatacho kwenye Mathayo 24:13 na Isaya 35:3, 4? (b) Tutabarikiwaje tukisonga mbele kwa muungano katika utumishi wa Yehova?
18 Yesu alisema: “Mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.” (Mathayo 24:13) Basi, tusiwe na “mikono iliyo dhaifu” au “magoti yaliyolegea” tungojapo siku ya Yehova iliyo kuu! (Isaya 35:3, 4) Unabii wa Sefania wasema hivi kwa kufariji kuhusu Yehova: “Shujaa awezaye kuokoa.” (Sefania 3:17) Ndiyo, Yehova ataokoa “umati mkubwa” kupita sehemu ya mwisho ya “dhiki ile iliyo kuu,” anapomwamuru Mwana wake kuvunja vipande-vipande mataifa ya kisiasa yanayoendelea “kujitukuza” juu ya watu wake.—Ufunuo 7:9, 14, NW; Sefania 2:10, 11; Zaburi 2:7-9.
-