-
“Fulizeni Kunitarajia”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
3 Jambo kuu ni kwamba ingawa Sefania alitangaza hukumu za kimungu dhidi ya “wakuu” wa kijamii wa Yuda (watu wenye vyeo vikubwa, au wakuu wa makabila) na “wana wa mfalme,” yeye hakutaja kamwe mfalme mwenyewe katika uchambuzi wake.a (Sefania 1:8; 3:3) Hilo ladokeza kwamba Mfalme Yosia mchanga tayari alikuwa ameonyesha mwelekeo mzuri kwa ajili ya ibada safi, ingawa, kwa kutazama hali iliyoshutumiwa na Sefania, kwa wazi hakuwa ameanza kufanya marekebisho yake ya kidini. Hayo yote yadokeza kwamba Sefania alitoa unabii katika Yuda katika miaka ya mapema ya Yosia, aliyetawala kuanzia 659 hadi 629 K.W.K. Unabii uliotolewa kwa bidii na Sefania bila shaka ulimsaidia Yosia mchanga kutambua kwamba ibada ya sanamu, jeuri, na ufisadi ulienea katika Yuda wakati huo na kutia nguvu kampeni yake ya baadaye dhidi ya ibada ya sanamu.—2 Mambo ya Nyakati 34:1-3.
-
-
“Fulizeni Kunitarajia”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
a Yaonekana kwamba maneno “wana wa mfalme” yarejezea wakuu wote wa kifalme, kwa kuwa wana wa Yosia mwenyewe walikuwa wachanga sana wakati huo.
-