Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Siku ya Hukumu ya Yehova I Karibu!
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Februari 15
    • 11. Ni nini maana ya andiko la Sefania 1:8-11?

      11 Kuhusu siku ya Yehova andiko la Sefania 1:8-11 laongeza kusema hivi: “Na itakuwa, katika siku ile ya dhabihu ya BWANA, nitawaadhibu wakuu, na wana wa mfalme, na watu wote waliovaa mavazi ya kigeni. Na katika siku ile nitawaadhibu hao wote warukao juu ya kizingiti, waijazao nyumba ya bwana wao udhalimu na udanganyifu. Na katika siku ile, asema BWANA kutakuwako sauti ya kilio kutoka lango la samaki, na mlio mkuu katika mtaa wa pili, na mshindo mkuu kutoka milimani. Haya! lieni, ninyi mkaao katika Makteshi, maana wafanya biashara wote wameangamia; hao wote waliokuwa na mizigo ya fedha wamekatiliwa mbali.”

  • Siku ya Hukumu ya Yehova I Karibu!
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Februari 15
    • 13. Kwa kupatana na unabii wa Sefania, ni nini ambacho kingetukia wakati Wababiloni wangeshambulia Yerusalemu?

      13 “Siku ile” ambayo Yuda ilitozwa hesabu yalingana na siku ya Yehova ya kutekeleza hukumu yake dhidi ya maadui wake, kukomesha uovu, na kuthibitisha ukuu wake. Wababiloni washambuliapo Yerusalemu, kilio kingetoka katika Lango la Samaki. Huenda liliitwa hivyo kwa kuwa lilikuwa karibu na soko la samaki. (Nehemia 13:16) Magenge ya Babiloni yangeingia sehemu iitwayo mtaa wa pili, na huenda ikawa “mshindo mkuu kutoka milimani” warejezea kishindo cha Wakaldayo wanaokaribia. Wakazi wa Makteshi, yamkini sehemu ya juu ya Bonde la Tiropoa, ‘wangelia.’ Kwa nini wangelia? Kwa sababu biashara, kutia ndani biashara ya “waliokuwa na mizigo ya fedha,” ingekoma.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki