-
“Fulizeni Kunitarajia”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
13. Sefania alitangaza ujumbe gani wenye hukumu dhidi ya Moabu, Amoni, na Ashuru?
13 Kupitia nabii wake Sefania, Yehova alionyesha hasira yake pia dhidi ya mataifa yaliyokuwa yamewatendea watu wake vibaya. Alitangaza hivi: “Mimi nimeyasikia matukano ya Moabu, na dhihaka za wana wa Amoni, ambazo kwa hizo wamewatukana watu wangu, na kujitukuza juu ya mpaka wao. Basi kama niishivyo, asema BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, Hakika Moabu atakuwa kama Sodoma, na wana wa Amoni kama Gomora, yaani, milki ya upupu, na mashimo ya chumvi, ukiwa wa daima. . . . Naye atanyosha mkono wake juu ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza Ashuru; naye ataufanya Ninawi kuwa ukiwa, kuwa mahali pakavu kama jangwa.”—Sefania 2:8, 9, 13.
14. Kuna uthibitisho gani kwamba mataifa ya kigeni ‘yalijitukuza’ juu ya Waisraeli na Mungu wao, Yehova?
14 Moabu na Amoni walikuwa maadui wa Israeli wa tangu zamani. (Linganisha Waamuzi 3:12-14.) Jiwe la Moabu, lililo katika Louvre Museum katika Paris, lina maandiko yenye taarifa ya kujisifu iliyotolewa na Mfalme Mesha wa Moabu. Yeye asimulia kwa majivuno jinsi alivyotwaa majiji kadhaa ya Israeli kwa msaada wa mungu wake Kemoshi. (2 Wafalme 1:1) Yeremia, aliyeishi wakati wa Sefania, alisema juu ya Waamoni kuwa wanakalia eneo la Israeli la Gadi katika jina la mungu wao Malkamu. (Yeremia 49:1) Kuhusu Ashuru, Mfalme Shalmanesa 5 alizingira na kuteka Samaria karibu karne moja kabla ya siku ya Sefania. (2 Wafalme 17:1-6) Baadaye kidogo, Mfalme Senakeribu alishambulia Yuda, akateka majiji mengi yenye ngome, na hata kutisha Yerusalemu. (Isaya 36:1, 2) Msemaji wa mfalme wa Ashuru alijitukuza juu ya Yehova alipokuwa akidai Yerusalemu lisalimu amri.—Isaya 36:4-20.
-
-
“Fulizeni Kunitarajia”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
15. Yehova angeaibishaje miungu ya mataifa yaliyojitukuza juu ya watu wake?
15 Zaburi 83 hutaja mataifa kadhaa, kutia ndani Moabu, Amoni, na Ashuru, waliojitukuza juu ya Israeli, na kusema hivi kwa kujigamba: “Njoni, tuwakatilie mbali wasiwe taifa, na jina la Israeli halitakumbukwa tena.” (Zaburi 83:4) Nabii Sefania alitangaza kwa moyo mkuu kwamba mataifa hayo yote yenye kiburi na miungu yayo yangeaibishwa na Yehova wa majeshi. “Mambo hayo yatawapata kwa sababu ya kiburi chao, kwa kuwa wamewatukana watu wa BWANA wa majeshi, na kujitukuza juu yao. BWANA atakuwa mwenye kuwatisha sana; kwa maana atawafisha kwa njaa miungu yote ya dunia; na watu watamsujudia yeye, kila mtu toka mahali pake; naam, nchi zote za mataifa.”—Sefania 2:10, 11.
-
-
“Fulizeni Kunitarajia”Mnara wa Mlinzi—1996 | Machi 1
-
-
17. Ni lini na ni jinsi gani jumbe zenye hukumu za Sefania zenye hukumu zilianza kutimizwa dhidi ya mataifa?
17 Wale waliotii onyo hilo hawakushangaa. Wengi waliishi wakaona utimizo wa unabii wa Sefania. Katika 632 K.W.K., Ninawi lilitekwa na kuharibiwa na muungano wa Wababiloni, Wamedi, na vikundi kutoka kaskazini, labda Waskaithia. Mwanahistoria Will Durant asimulia: “Jeshi la Wababiloni chini ya Nabopolasari liliungana na jeshi la Wamedi chini ya Siaksaresi na vikundi vya Waskaithia kutoka Kaukasi, na kwa urahisi na wepesi wenye kushangaza waliteka ngome za kaskazini. . . . Kwa pigo moja Ashuru ilipotea katika historia.” Hivyo ndivyo alivyotabiri Sefania.—Sefania 2:13-15.
-