Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 5. Ni nini uthibitisho wa kwamba kitabu cha Hagai chafaa kuwa katika vitabu vinavyokubaliwa vya Biblia?

      5 Hakukuwa na shaka kamwe miongoni mwa Wayahudi juu ya kama unabii wa Hagai ulikuwa sehemu ya vitabu vya Kiebrania vilivyokubaliwa, na jambo hilo laungwa mkono pia na kurejezewa kwake katika Ezra 5:1 kuwa akitoa unabii “kwa jina la Mungu wa Israeli,” na pia katika Ezra 6:14. Kwamba unabii wake ni sehemu ya “kila andiko, lenye pumzi ya Mungu” yathibitishwa na kunukuliwa kwao na Paulo kwenye Waebrania 12:26: “Sasa ameahidi akisema, Mara moja tena nitatetemesha si nchi tu, bali na mbingu pia.”—Hag. 2:6.

  • Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 10. Wayahudi fulani wahisi nini juu ya hekalu wanalojenga, lakini Yehova aahidi nini?

      10 Ujumbe wa pili (2:1-9). Muda unaopungua mwezi mmoja wapita baada ya kuanzishwa tena kwa utendaji wa kujenga, na Hagai atoa ujumbe wake wa pili wenye pumzi ya Mungu. Huo umeelekezwa kwa Zerubabeli, Yoshua, na waliobaki wa watu hao. Kwa wazi baadhi ya Wayahudi waliorudi kutoka uhamishoni na waliokuwa wameona hekalu la kwanza la Sulemani walihisi kwamba hekalu hili halingekuwa kitu likilinganishwa na hilo jingine. Lakini ni nini tangazo la Yehova wa majeshi? ‘Mwe hodari, mkafanye kazi, kwa kuwa mimi ni pamoja nanyi.’ (2:4) Yehova awakumbusha agano lake pamoja nao, na kuwaambia wasiogope. Awaimarisha kwa ahadi ya kwamba atatikisa mataifa yote na kusababisha vitu vyayo vyenye kutamanika vije ndani na kwamba atajaza nyumba yake utukufu. Utukufu wa nyumba hii ya baadaye utakuwa mkubwa hata kuliko ule wa ile ya kwanza, na yeye atatia amani katika mahali hapa.

  • Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 16. Unabii wa Hagai una uhusiano gani na tumaini la Ufalme, nao wapasa kutuchochea kwenye utumishi gani leo?

      16 Vipi juu ya unabii wa kwamba Yehova ‘atatikisa mbingu na nchi’? Mtume Paulo atoa matumizi ya Hagai 2:6 katika maneno haya: “Lakini sasa [Mungu] ameahidi akisema, Mara moja tena nitatetemesha si nchi tu, bali na mbingu pia. Lakini neno lile, Mara moja tena, ladhihirisha kuhamishwa vile viwezavyo kutetemeshwa, kama vitu vilivyoumbwa, ili vitu visivyoweza kutetemeshwa vikae. Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na tuwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho; maana Mungu wetu ni moto ulao.” (Ebr. 12:26-29) Hagai aonyesha kwamba kutikiswa huko ni kwa kusudi la ‘kupindua kiti cha enzi cha falme, na kuharibu nguvu za falme za mataifa.’ (Hag. 2:21, 22) Katika kunukuu unabii huo, Paulo anena kwa kutofautisha, juu ya Ufalme wa Mungu “usioweza kutetemeshwa.” Basi kwa kufikiria tumaini hili la Ufalme, acheni tuwe ‘hodari tukafanye kazi,’ tukitolea Mungu utumishi mtakatifu. Pia, na tufikirie kwamba kabla Yehova hajapindua mataifa ya dunia, kitu fulani chenye thamani lazima kikorogwe kitoke kwayo, kwa ajili ya kuhifadhiwa: “Nami nitatikisa mataifa yote, na vitu vinavyotamaniwa na mataifa yote vitakuja; nami nitaijaza nyumba hii utukufu, asema BWANA [Yehova, NW] wa majeshi.”—2:4, 7.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki