Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 11. (a) Ni kwa kutumia ufananishi gani Hagai aonyesha wazi kutojali kwa makuhani? (b) Ni nini kimetokana na jambo hilo?

      11 Ujumbe wa tatu (2:10-19, NW). Miezi miwili na siku tatu baadaye, Hagai asema kwa makuhani. Atumia ufananishi ili kuelewesha wazi wazo lake. Je! kuchukua kwa kuhani mnofu mtakatifu kutafanya chakula kingine chote anachogusa kiwe kitakatifu? Jibu ni la. Je! kugusa kitu kisicho safi, kama vile maiti, kwafanya mwenye kuigusa awe si safi? Jibu ni ndiyo. Ndipo Hagai anapotumia ufananishi huo. Watu wa bara lile si safi kwa sababu ya kutojali kwao ibada yenye kutakata. Chochote wanachotoa chaonekana si safi kwa Yehova Mungu. Kwa sababu hiyo, Yehova hakubariki kazi zao za jasho, na kuongezea hilo amewapelekea joto lenye kuchoma sana, kuvu, na mawe ya mvua. Acha wao wabadili njia zao. Kisha Yehova atawabariki.

  • Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
    • 14. Hagai atoa shauri gani lenye hekima kwa ajili ya siku yetu?

      14 Pia unabii huo una shauri la hekima kwa ajili ya siku yetu. Vipi? Jambo moja ni kwamba wakazia uhitaji wa kiumbe kutanguliza faida za ibada ya Mungu mbele ya faida za kibinafsi zacho chenyewe. (Hag. 1:2-8; Mt. 6:33) Pia wakazia jambo la kwamba ubinafsi waleta hasara, kwamba ni ubatili kufuatia mali; amani na baraka ya Yehova ndizo hutajirisha. (Hag. 1:9-11; 2:9; Mit. 10:22) Pia wakazia kwamba utumishi wa Mungu wenyewe haumfanyi mtu kuwa safi isipokuwa uwe watakata na wa nafsi yote, na kwamba haupaswi kunajisiwa kwa mwenendo mchafu. (Hag. 2:10-14; Kol. 3:23; Rum. 6:19) Waonyesha kwamba watumishi wa Mungu hawapaswi kuwa na maoni yasiyofaa, wakitazama nyuma “siku njema zilizopita,” bali wawe wenye kutazama mbele, ‘wakitafakari njia zao’ na kutafuta kuletea Yehova utukufu. Kisha Yehova atakuwa pamoja nao.—Hag. 2:3, 4; 1:7, 8, 13; Flp. 3:13, 14; Rum. 8:31.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki