-
Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
3. Wayahudi walikuwa wamekosa kujua nini kwa habari ya kusudi la kurudi kwao kutoka uhamishoni?
3 Kwa nini Yehova alimpa Hagai utume? Kwa sababu hii: Katika 537 K.W.K., Koreshi alikuwa ametoa amri iliyoruhusu Wayahudi warudie bara la kwao kujenga upya nyumba ya Yehova. Lakini sasa ilikuwa 520 K.W.K., na hekalu lilikuwa mbali na kukamilishwa. Muda wa miaka yote hiyo Wayahudi walikuwa wameacha vipingamizi vya adui pamoja na ubaridi wao wenyewe na ufuatiaji vitu vya kimwili uwazuie kutimiza kusudi lenyewe la kurudi kwao.—Ezra 1:1-4; 3:10-13; 4:1-24; Hag. 1:4.
-
-
Kitabu Cha Biblia Namba 37—Hagai“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
-
-
8. Kwa nini Wayahudi hawabarikiwi na Yehova kwa vitu vya kimwili?
8 Ujumbe wa kwanza (1:1-15). Huu waelekezwa kwa Liwali Zerubabeli na Kuhani Mkuu Yoshua, lakini masikioni mwa watu hao. Watu hao wamekuwa wakisema, “Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujengwa nyumba ya BWANA [Yehova, NW].” Kupitia Hagai Yehova auliza swali la kupekua-pekua maoni: “Je! huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?” (1:2, 4) Wao wamepanda mbegu nyingi kwa kufuatia vitu vya kimwili, lakini hawakunufaika sana kwa njia ya chakula, kinywaji, na nguo. “Zitafakarini njia zenu,” Yehova aonya kwa upole. (1:7) Wakati umefika wa kuleta mbao na kujenga nyumba ile, ili Yehova apate kutukuzwa. Wayahudi watunza vizuri nyumba zao wenyewe, lakini nyumba ya Yehova imelala hali ya ukiwa. Kwa hiyo, Yehova amekuwa mnyimivu ili umande wa mbinguni na ongezeko la shambani na baraka yake visiwe juu ya mwanadamu na jasho lake.
-