-
“Tutakwenda Pamoja Nanyi”Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2016 | Januari
-
-
1, 2. (a) Yehova alisema ni nini ambacho kingetokea wakati wetu? (b) Makala hii itajibu maswali gani? (Tazama picha mwanzoni mwa makala hii.)
YEHOVA alitabiri hivi kuhusu wakati wetu: “Na itakuwa katika siku hizo kwamba watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa watashika, ndiyo, wataushika upindo wa nguo ya mtu aliye Myahudi, wakisema: ‘Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu yupo pamoja nanyi.’” (Zek. 8:23) Kama watu hao kumi wa mfano, wale wenye tumaini la kuishi duniani ‘wameushika upindo wa nguo ya Myahudi.’ Wanajivunia kushirikiana na wale waliotiwa mafuta kwa roho, yaani “Israeli wa Mungu,” wakijua kwamba Yehova anawabariki watiwa mafuta hao.—Gal. 6:16.
-
-
“Tutakwenda Pamoja Nanyi”Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2016 | Januari
-
-
4. Ikiwa haiwezekani kujua majina ya watiwa mafuta wote walio duniani leo, tunawezaje ‘kwenda pamoja nao’?
4 Ikiwa haiwezekani kujua kikamili majina ya Waisraeli wote wa kiroho walio duniani leo, kondoo wengine wanawezaje ‘kwenda pamoja nao’? Fikiria kile ambacho nabii Zekaria anasema kuhusu watu kumi wa mfano. Watu hao “wataushika upindo wa nguo ya mtu aliye Myahudi, wakisema: ‘Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu yupo pamoja nanyi.’” Ingawa ni Myahudi mmoja tu anayetajwa katika unabii huo, neno “nanyi” linawakilisha mtu zaidi ya mmoja. Hivyo, Myahudi wa kiroho anayetajwa hapo si mtu mmoja bali ni kikundi cha watu. Kwa hiyo, si lazima tumjue kila Myahudi wa kiroho na kwenda pamoja naye. Badala yake, tunapaswa kuwatambua wakiwa kikundi na kisha tuwaunge mkono. Maandiko hayatutii moyo kamwe tumfuate mtu fulani. Kiongozi wetu ni Yesu.—Mt. 23:10.
-