-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
12. Ni kwa nini washiriki wa sinagogi la Kiyahudi katika Filadelfia inaelekea wangeshtuka kujifunza kwamba baadhi yao ‘wangeinamia’ jamii ya Kikristo ya mahali hapo?
12 Washiriki wa Sinagogi la Kiyahudi katika Filadelfia inaelekea wangeshtuka kujifunza kwamba baadhi yao ‘wangesujudia’ jamii ya Kikristo ya mahali hapo. Kwa sababu ya uhakika wa kwamba bila shaka kuna wasio Wayahudi wengi katika kundi hilo, wao wangetazamia jambo lililo kinyume kabisa litukie. Kwa nini? Kwa sababu Isaya alitabiri hivi: “Wafalme [wasio Wayahudi] lazima wawe watunzi kwa ajili yako wewe [watu wa Israeli], na mabinti-wafalme wao wanawake wa kulea kwa ajili yako wewe. Nyuso zikiwa kwenye dunia watainama mbele yako wewe.” (Isaya 49:23, NW; 45:14; 60:14) Katika maana iyo hiyo, Zekaria alivuviwa kuandika hivi: “Itakuwa siku hizo kwamba wanaume [wasio Wayahudi] kumi kutoka lugha zote za mataifa watashika, ndiyo, hakika watashika rinda la mwanamume aliye Myahudi, wakisema: ‘Sisi tutaenda na nyinyi watu, kwa maana sisi tumesikia kwamba Mungu yu pamoja na nyinyi watu.’” (Zekaria 8:23, NW) Ndiyo, watu wasio Wayahudi wangeinamia Wayahudi, si kinyume cha hivyo!
-
-
“Fuliza Kushikilia kwa Imara Kile Ulicho Nacho”Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
14. Ni jinsi gani Isaya 49:23 na Zekaria 8:23 yamekuwa na utimizo wa maana katika nyakati za ki-siku-hizi?
14 Katika nyakati za ki-siku-hizi, unabii kama vile Isaya 49:23 na Zekaria 8:23 umekuwa na utimizo wenye umaana sana. Likiwa tokeo la kuhubiri kwa jamii ya Yohana, hesabu kubwa za watu zimepitia ule mlango uliofunguliwa wakaingia ndani ya utumishi wa Ufalme.b Walio wengi wa hawa wametoka katika Jumuiya ya Wakristo, ambayo dini zayo hudai kwa ubandia kuwa Waisraeli wa kiroho. (Linga Warumi 9:6.) Hawa, wakiwa umati mkubwa, wanafua mavazi yao na kuyafanya meupe kwa kutumia imani katika damu ya dhabihu ya Yesu. (Ufunuo 7:9, 10, 14) Kwa kutii utawala wa Kristo wa Ufalme, wanatumaini kurithi baraka zao hapa duniani. Wanakuja kwa ndugu za Yesu wapakwa-mafuta na ‘kuwainamia,’ kiroho, kwa sababu ‘wamesikia kwamba Mungu yu pamoja nao.’ Wanahudumia hawa wapakwa-mafuta, ambao pamoja nao wanakuwa wenye umoja katika ushirika wa ndugu ulimwenguni pote.—Mathayo 25:34-40; 1 Petro 5:9.
-